HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

August 14, 2013

UCHAGUZI MKUU WA TFF SASA OKTOBA 20

Rais anayemaliza muda wake, Leodegar Tenga.

DAR ES SALAAM, Tanzania

KAMATI ya Uchaguzi ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), imetangaza tarehe ya Uchaguzi Mkuu wa TFF na ule wa Bodi ya Ligi Kuu (TPL Board), mchakato unaoanzia keshokutwa Agosti 16 kwa wagombea kuchukua fomu kuwania nyadhifa mbalimbali.

Akizungumza jijini Dar es Salaam leo, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Hamidu Mbwezeleni, alisema kuwa Uchaguzi wa Bodi ya TPL, utafanyika Oktoba 18, siku mbili kabla ya kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu wa TFF, Oktoba 20, badala ya Septemba 29 ya awali.

Mbwezeleni alibainisha kuwa, nafasi zitakazogombewa katika uchaguzi wa TFF ni Rais, Makamu wake na Wajumbe 13 wa Kamati ya Utendaji, watakaowakilisha kanda tofauti, huku uchaguzi wa Bodi ya TPL ikiwa ni nafasi ya Mwenyekiti, Makamu na Wajumbe wa bodi hiyo.

Akizungumzia mchakato huo uliosimamishwa awali na Fifa, Mbwezeleni alisisitiza kuwa, wagombea wanapaswa kuzijua sheria na kanuni zinazosimamia uchaguzi huo zinazopatikana katika ‘Election Menu’ ya TFF, ili kujua miongozo na taratibu ili kuondoa malalamiko.

No comments:

Post a Comment

Pages