HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

December 21, 2013

WAIMBAJI TAMASHA LA KRISMASI WAANZA KUTUA
Na Mwandishi Wetu

WAIMBAJI wa kimataifa wa nyimbo za injili ambao watahudumu katika Tamasha la Krismasi litakalozinduliwa Desemba 25 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, wameanza kuwasili tayari kuwapa raha wapenzi, mashabiki na wadau.

Akithibitisha hilo, Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Tamasha hilo la kimataifa, Alex Msama (pichani), alisema waimbaji ambao wameshatua jijini Dar es Salaam ni Ephraim Sekeleti kutoka Zambia na Solomoni Mkubwa kutoka Kenya.

Msama alisema kuwasili kwa waimbaji hao ni faraja kubwa kwa kamati yake kwani ni mwanzo wa wengine kuanza kuwasili kutoka Afrika Kusini na Rwanda.

Alisema mbali ya hao wa kigeni, Malkia wa nyimbo za Injili Tanzania, Rose Muhando aliyekuwa nje ya nchi, amerejea naye yupo jijini Dar es Salaam katika maandalizi ya mwisho kuelekea tamasha hilo ambalo baada ya kuziduliwa uwanja wa Taifa, mashambulizi yataendelea mikoani hadi Januari mosi.

Msama alisema baada ya tamasha hilo kuzinduliwa Uwanja wa Taifa, mashambulizi yatahamia jijini Arusha, Morogoro na Dodoma.
Kuhusu tiketi za tamasha hilo, Msama alisema zitauzwa katika maduka ya Msama Promotions yaliyoko Mtaa wa Mkwepu, Posta na Kariakoo, mtaa wa Masasi na Msimbazi  karibu na Kanisa la Lutherani.

Maeneo mengine ni vituo vya mafuta vya Puma Mwenge, Tangibovu na uwanja wa ndege, Best bite Namanga, ofisi za Msama Promotions, Kinondoni Biafra, Wapo Radio na Praise Power redio.
Viingilio kwa VIP A ni sh 20,000, VIP B ni sh 10,000, mzunguko ni sh 5,000 na watoto sh 2000 na  mikoani ni sh 5,000 kwa wakubwa na watoto sh 2000.

1 comment:

  1. Samahani ninashindwa kuelewa...Kama timu ya Simba wamewafunga Yanga inakuwaje wao (Simba) wapate TShs 1m na Yanga waliofungwa wapate TShs 98m? Naomba ufafanuzi, tafadhali.

    ReplyDelete

Pages