HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

January 07, 2014

MAGONJWA YASIYOAMBUKIZWA HATARI ZAIDI KWA VIJANA
  Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Hamis Mdee  akipima afya yake kwenye banda ya NHIF katika maonesho ya maadhimisho ya miaka 50 ya Mapinduzi Zanzibar.
 Mwakilisho wa NHIF Zanzibar Ismail Kangeta (Katikati) akitoa elimu ya umuhimu na namna ya kujiunga na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya katika maonesho hayo.
 Ofisa Elimu kwa Umma wa NHIF, Grace Michael akifafanua jambo kwa wananchi waliofika katika banda la Mfuko huo.
 Wananchi wakiendelea kupata huduma ya kupima afya zao ikiwemo uzito na hatimaye kupata elimu ya kujikinga na maradhi yasiyoambukiza.
 Ofisa wa NHIF katika ofisi ya Zanzibar, Shaaban Mhunzi akitoa huduma kwa wananchi waliofika bandani hapo.
Bi. Asha Alli akipima sukari na kupata ushauri wa kitaalam kutoka kwa mtaalam Khamis Haji Haji.
Kaimu Mkurugwenzi Mkuu wa NHIF, Hamis Mdee akibadilishana mawazo na mwakilishi wa Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam Dennis Madaha wakati wa maonesho hayo.
Ofisa Masoko na Elimu kwa Umma Catherine Kameka akitoa elimu kwa wananchi waliofika bandani hapo. (PICHA ZOTE NA IDARA YA MASOKO NA ELIMU KWA UMMA NHIF)


Na Irene Mark, aliyekuwa Zanzibar

VIJANA wengi wenye umri kati ya miaka 30 na 40 wanakabiliwa na tatizo la uzito uliozidi hali inayowaweka kwenye hatari ya kupata magonjwa yasiayoambukizwa.

Akizungumza wakati wa maonyesho ya kuadhimisha miaka 50 ya Mapunduzi Zanzibar, Ofisa Uhakiki Ubora wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Dk. Ally Mvita alisema hiyo ni hatari kwa taifa.

Kwa mujibu wa Dk. Mvita magonjwa yasiyoambukizwa yanayotokana na uzito wa mwili kuzidi ni Kisukari na Shinikizo la Damu ambayo hudhoofisha nguvukazi ya mgonjwa na kuzorotesha maendeleo binafsi na taifa.

“Katika kipindi cha siku nne za maonyesho haya tumewapima bure wananchi zaidi ya 700 wengi ni vijana wenye umri kati ya miaka 30 na 40 ambao asilimia zaidi ya 75 ya vijana hao tumegundua kwamba wanauzito uliozidi.

“Kitaalam tunaita ‘over weight’ na ‘obesity’ uwiano wa urefu na uzito kiafya havilingani, hii ni hatari kwa sababu ni rahisi mtu huyo kupata kisukari na shinikizo la damu,” alisema Dk. Mvita.

Aidha aliwashauri watu wenye matatizo hayo kufanya mazoezi na kupunguza ulaji wa vyakula bila mpangilio ili kujiepusha na magonjwa hayo.

Maonyesho hayo yalimalizika Januari 5 mwaka huu kwenye viwanja vya Betras, mjini Unguja ambapo viongozi mbalimbali wa Serikali ya Mapinduzi (SMZ) na ile ya Muungano walitembelea banda la NHIF na kupima afya zao.

No comments:

Post a Comment

Pages