NA ELIZABETH JOHN
MKALI wa muziki wa kizazi kipya nchini,
Abdul Sykes ‘Dully Sykes’ amesema
imepita miaka miwili hajawahi kupigiwa simu na promota yeyote nchini
kwaajili ya kufanya shoo.
Akizungumza na mtandao wa Bongo5, jijini
Dar es Salaam jana, Dully alisema hiyo imetokana nay eye mwenyewe kutojiweka
sokoni na kuamua kufanya kazi za utayarishaji wa muziki huo.
Alisema kuwa, hawezi kufanya shoo kwa bei
ambayo yeye haitaki ila shoo yake yeyote anataka aingize zaidi ya milioni kumi.
“Shoo zangu nyingi sifanyi chini ya milioni
kumi, hivyo anaenihitaji ajue nataka nini sio kuniita kwa bei za mtaani na
kupotezeana muda, kila msanii anamalengo yake hivyo siwezi kukurypuka na kutaka
shoo kwa bei ambayo itaniumiza mwenyewe,” alisema.
Dully alishawahi kutamba na vibao vyake
kama, Salome, Kabinti Special, Mtoto wa Kariakoo, Dhahabu na nyinginezo nyingi
ambazo zilimtambulisha na kufanya vizuri katika tasnia ya muziki huo.
No comments:
Post a Comment