HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

August 28, 2014

PRODUCER NAH REEL AFUNGUA STUDIO DAR


NA SYLVESTER DAVID


MTAYARISHAJI na msanii maarufu wa muziki nchini,Emanuel Mkono, ‘Nah Reel’amefungua studio ya kufanyia muziki  yenye lengo la kusaidia  kuboresha kazi za wasanii .
 

Akizungumza katika studio yake Mwenge jijini Dar es salaam, alisema amefungua studio yake binafsi inayojulikana kwa jina la ‘The Industry’ kutokana na kukosa muda wa kutosha wa kufanya kazi nyingi hii ni   kutokana na kupekezana majukumu baina ya watayarishaji wenzake katika studio aliyokuwa akifanya awali .


Nah Reel ambaye amewahi kuwa mtayarishaji wa muziki katika studio mbalimbali nchini zikiwemo Kama Kawa Record,Home Town Record,Switch Record na The Industy na kufanya nyimbo kama,Tanzania ya Roma Mkatoriki,Wimbo Wa Taifa ya Kalla Jelemaya, Niaje Nivipi ya Nick wa 2,Come Over ya Vanesa Mdee , Mfalme ya Mwana Fa,Ridhiwan Ya Izzo Busness,Nyimbo zote za kundi la Weusi na Navy Kenzo na nyinginezo kibao.


“Nimeamua kufungua studio yangu kutokana na ndoto zangu tokea zamani za kumiliki  studio vilevile kuwa na muda mwingi wa kufanya kazi zangu kutokana na mahitaji ya watu kwa muziki wangu na kusaidia kuboresha muziki nchini”, alisema


Vile vile Nah Real alikanusha kauli ya msanii Hamis Mwinjuma ‘Mwana Fa’ kutokana na kwamba wimbo wake wa ‘Mfalme’,kuwa umeandaliwa na Marco Chali kwa kushirikiana na mwandaaji huyo  akiwa katika mahojiano vyombo mbalimbali vya habari wakati ukweli ni kwamba wimbo huo umeandaliwa na Nahreal nba hatua za mwisho kufanya na Marco Chali.


Aliongeza kwa kuwataka wasanii pamoja na waandaji wa muziki  kuwa na sera madhubuti za kulinda kazi ili ziwafaidishe bila kutegemea serikali. Email:silvesterhabari@gmail.com
0715-577805

                              

No comments:

Post a Comment

Pages