HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

August 25, 2014

RAIS SHEIN AWAAPISHA MAWAZIRI, WAKUU WA WILAYA WAPYA IKULU LEO

  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi  Dk.Ali Mohamed Shein akimuapisha Dk.Sira Ubwa  Mamboya kuwa Waziri wa Kilimo na Maliasili katika Ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar kabla Dk.Sira alikuwa Naibu Waziri wa Afya. (Picha na Ramadhan Othman Ikulu)
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi  Dk.Ali Mohamed Shein akimuapisha Juma Duni Haji  kuwa Waziri wa  Miundombinu na Mawasiliano katika Ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar kabla alikuwa  Waziri wa Afya.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi  Dk.Ali Mohamed Shein akimuapisha Rashid  Seif Suleiman kuwa Waziri wa Afya,awali alikuwa Waziri wa   Miundombinu na Mawasiliano hafla ya kiapo imefanyika katika Ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar leo.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi  Dk.Ali Mohamed Shein akimuapisha Mahmoud Thabit Kombo  kuwa Naibu Waziri wa Afya, hafla ya kiapo imefanyika katika Ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar leo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi  Dk.Ali Mohamed Shein akimuapisha Meja mstaafu Juma Kassim Tindwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja.

  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi  Dk.Ali Mohamed Shein akimuapisha Bw. Omar Khamis Othman kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini  Pemba.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi  Dk.Ali Mohamed Shein akimuapisha Mwanajuma Majid Abdulla kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba katika ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar leo, kabla alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Chake Chake Pemba.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi  Dk.Ali Mohamed Shein akimuapisha Bw. Ayoub Mohamed Mahmoud kuwa Mkuu wa Wilaya Magharibi  leo katika ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar,awali alikua Afisa Tawala katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mjini magharibi Unguja.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi  Dk.Ali Mohamed Shein akimuapisha Bibi Hanuna Masoud Ibrahim kuwa Mkuu wa Wilaya ya  Chake chake Pemba.

No comments:

Post a Comment

Pages