HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

August 17, 2014

Rais Kikwete ahudhuria Mkutano wa 34 wa SADC Victoria Falls

 Rais Dkt. Jakaya Kikwete akipokea maua kutoka kwa watoto leo muda mfupi baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa mji wa Victoria Falls  nchini Zimbabwe ambapo atashiriki katika mkutano wa 34 wa siku mbili wa wakuu wa nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika SADC. (Picha na Freddy Maro)
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na Rais Hifikepunye Pohamba wa Namibia muda mfupi kabla ya kuanza kwa mkutano wa 34 wa wakuu wa nchi za SADC unaofanyika katika mji wa Victoria Falls nchini Zimbabwe.
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete,Rais Hifikepunye Pohamba wa Namibia na Rais Jackob Zuma wa Afrika ya kusini wakijadiliana jambo kabla ya kuanza kwa mkutano wa 34 wa wakuu wa nchi za SADC unaofanyika katika hoteli ya Elephant Hills, mjini Victoria Falls nchini Zimbabwe.

No comments:

Post a Comment

Pages