HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

August 15, 2014

SERIKALI YATAKIWA KUPUNGUZA BAJETI ZA WIZARA

Baadhi ya wajawazito wakiwa wamekaa chini kutokana na uhaba wa vitanda.


NA SYLVESTER DAVID
TAASISI isiyo ya kiserikali ya Society Watch,imeishauri serikali kupunguza  gharama za uendeshaji wa Ofisi za wizara badala yake zitumike kuwasaidia wajawazito masikini nchini..

Hayo yalisemwa jana na Mtendaji Mkuu wa taasisi  hiyo, Simon Nkondya katika mahojiano maalumu jijini Dar es salaam.
Nkondya ambaye ni mwanaharakati wa kutetea haki za akina mama wajawazito alisema wameamua kukusanya maoni kutoka kwa wadau mbalimbali wakiwemo watumishi wa afya, serikali na viongozi wa taasisi binafsi kutokana na kuguswa na hali hiyo na kuendelea kutafuta jitihada za kuinusuru unyanyasaji wa wanawake na miundombinu za kuwafikisha  katika hospitali mbalimbali.
“Kama viongozi wetu wakitumia magari ya serikali yenye gharama ya shilingi million 15 yatafanya pesa zingine kutumika katika huduma mbalimbali za kijamii ikiwezekana kuboresha huduma kwa wajawazito tofauti na tafiti zinavyoonyesha kuwa wanatumia gari za shilingi million 300”,alisema
Aliongeza kuwa, Taasisi ya Society Watch linatarajia kuandaa tamasha la wajawazito nchini ifikapo Desemba 14 mwaka huu ,Kuongeza  juu ya ujauzito, kupunguza vifo kwa wajawazito na watoto chini ya miaka mitano, kupunguza mimba za utotoni, kukuza uzalendo na kuhamasisha wajawazito kupenda kujifungulia kwenye vituo vya Afya-serikali.

Pia aliongeza kuwa taasisi imefanya tukio la kuhesabu mashimo ya barabara kutokea Tabata Kimanga mpaka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa kutumia fimbo ya Society Watch yenye ujumbe mbalimbali za harakati za haki za binadamu lengo ni kujua adha na mitikisiko inayoweza kuharibu ujauzito waipatayo wawapo barabarani na kugundua kuna idadi ya mashimo 27,253  , ambayo ni hatari kwa afya za wajawazito.

No comments:

Post a Comment

Pages