HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

October 18, 2014

Bayport Tanzania yazindua huduma mpya ya Mikopo ya bidhaa



 Meneja wa Masoko na mawasiliano wa taasisi ya kifedha ya Bayport Tanzania, Ngula Cheyo (katikati) akiongea na wandishi wa habari (Hawapo pichani) wakati wa utambulisho wa huduma ya Mikopo ya bidhaa.

Meneja wa Masoko na mawasiliano wa taasisi ya kifedha ya Bayport Tanzania, Ngula Cheyo (wa kwanza kushoto),  akifuatiwa na Meneja masoko wa Toyo,  Drima Makachwa (katikati)  pamoja na  Meneja Bishara wa Bayport, Thabit Mndeme (kulia), kwenye uzinduzi huo.


Na Andrew Chale

Taasisi ya kifedha ya Bayport Tanzania  mapema leo Oktoba 15, 2014 imezindua huduma mpya ijulikanayo kama Mikopo ya bidhaa ikiwa na lengo la kurahisisha utendaji kazi wa watumishi wa umma na wafanyakazi wote wa kampuni zilizoidhinishwa na Bayport.

Uzinduzi  huo ulifanyika katika ofisi za makao makuu ya Bayport, maeneo ya Moroco jijini Dar es Salaam mbele ya wandishi wa vyombo mbalimbali vya habari  umeonyesha matumaini mapya ya watanzania wanaosumbukia usafiri katika vituo vyao vya kazi, hususani maeneo ya mikoani ambako mara kadhaa kumesikika malalamiko ya maisha magumu kwa watumishi wa umma.

Akizungumza juu ya tukio hilo, Meneja Bishara wa taasisi hiyo Thabit Mndeme alisema kwamba ni wakati wa kukuza uchumi wa nchi kuhakikisha kuwa watu wanafanya kazi kwa bidii na shauku.
Alisema wapo watumishi ambao wanaishi kwa tabu kutokana na changamoto ya usafiri na mahitaji mengine ya kijamii ,hivyo kutokana na huduma hiyo mpya ya kukopeshwa pikipiki ,boda boda itasaidia kwa kiasi chake.

Pia alisema Bay port imekaa kuangalia namna ganib watanzania wataendelea kufanya kazi kwa moyo na kukuza uchumi ambao uko sambamba na kuwakopesha  fedha kama wanavyofanya kwa sasa na kuamua kuwakopesha tena na bidhaa za usafiri.

Naye Meneja wa Masoko na mawasiliano wa taasisi hiyo Ngula Cheyo alisema kuwa mikopo mipya kwa sasa inapatikana kwa masaa 24, huku ikipatikana pia kwa mikoa na wilaya zote kwenye ofisi za Bayport zaidi ya 80, nchini.

Bayport ni Taasisi ya kifedha isiyo ya kibenki inayoongoza katita utowaji wa mikopo barani Africa na Amerika ya kusini .imeanzishwa mwaka 2001, na umiliki wake ukiwa Mauritius.

No comments:

Post a Comment

Pages