HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

October 16, 2014

Kasisi alia na Katiba, adai inasumbua sababu hakuna Upendo


Na Bryceson Mathias, Chibelela, Bahi

KASISI Ujumla (Vicar General), George Chomola, wa Kanisa la Anglikani Dayosisi ya Central Tanganyika (DCT) Dodoma, ameililia Katiba Mpya akisema inasumbua kwa sababu hakuna Upendo miongoni mwa Watendaji wake.

Akizungumza katika Msiba wa Mjumbe wa Halmashauri Kuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) NEC, Ernest Masima, aliyezikwa nyumbani kwake katika kijiji cha Chibelela mkoani Dodoma mwishoni mwa Wiki, Chomola amesema, Katiba Mpya inasumbua kwa sababu hakuna Upendo.

Ingawa Chomola hakutaka kuingia ndani ili kufafanua upendo unaokosekana kwenye Katiba mpya inayopendekezwa, lakini Mizengwe, Kukosekana Maridhiano, Vituko na Udanganyifu uliokithiri katika upigaji kura wa Bunge Maalum la Katiba kutafuta Theluthi Mbili ni mojawapo.

Mbali na kwamba Msiba huo ulikiumiza CCM kwa jinsi Kada wake Marehemu Ernest alivyokitumikia na kukisaidia kufanya Mengi ikiwa ni pamoja na Ushauri akiwa Mkuu wa Wilaya na kazi zingine katika sehemu mbalimbali, CCM isifadhaike, Mungu amempenda zaidi.

Kasisi Chomola alinukuu Neno la Mungu la Yohana 14:1-2 kuwafariji CCM, Ndugu na Waombolezaji linalosema, “Msifadhaike mioyoni mwenu; mnamwamini Mungu, niaminini na mimi.Nyumbani mwa Baba yangu mna makao mengi; kama sivyo, ningaliwaambia………;”

Kwetu sisi kwa Upande wa Kanisa tuna Majonzi Makubwa kwa sababu alikuwa Kiongozi wa Shughuli mbalimbali za Kanisa ikiwa ni pamoja na Ujenzi wa Kanisa la Anglikani hapa Chibelela, lakini bado nasema Mungu anasema, ‘Msifadhaike’”.alisema Chomola.

Hata hivyo, Chomola Kabla ya kutoa Mahubiri, alimkaribisha Katibu wa CCM Mstafu Yusuf Makamba ili aelezee anavyomfahamu Marehemu, lakini alimpiga ‘Stop’ asije akaanza sihubiri, akidai hasa kutokana na kwamba anafahamu vifungu vingi vya Neno la Mungu.

No comments:

Post a Comment

Pages