HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

October 01, 2014

Serikali yashauriwa kufuta ada shule za kata

KAIMU Ofisa wa Ustawi wa Jamii Mkoa wa Pwani, Dismas Chuwalo, ameishauri serikali kufuta ada ya shule za sekondari za Kata ili wahitimu wote wanaochaguliwa waweze kujiunga na shule hizo.

Chuwalo, alitoa kauli hiyo wakati wa mahafali ya pili ya shule ya msingi Calvary Montesori, yaliyofanyika jijini Dar es Salaam.

Alisema wazazi wengi waliopo maeneo ya vijijini wanashindwa kuwapeleka watoto wao kujiunga na kidato cha kwanza katika shule hizo kutokana na kushindwa kulipa ada na michango mingine mbalimbali.

Aliwataka wazazi kuhakikisha wanatenga muda wa kufuatilia maendeleo ya watoto wao, ikiwa ni pamoja na kukagua madaftari.

Mkurugenzi wa Shule hiyo, Sibonike Mponzi, alisema ya shule hiyo imekuwa na mafanikio ya kitaaluma kutokana na uongozi kutoa motisha kwa walimu kila mwaka tangu ilipoanzishwa.

Alisema ili shule za serikali zifanye vizuri katika ufaulu, ni vema ikawapatia walimu motisha na kuwajengea mazingira bora ya kazi katika shule wanazofundisha.

No comments:

Post a Comment

Pages