HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

November 04, 2014

NSSF YADHAMINI MASHINDANO YA SHIMISEMITA MKOANI MOROGORO

Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) ndio mdhamini Mkuu wa mashindano ya Shirikisho la Michezo Serikali za Mitaa (Shimisemita) inayoendelea katika Uwanja wa Jamhuri mkoani Morogoro  hadi Novemba 11.

 Katika mashindano hayo NSSF imepata fursa ya kutoa elimu kuhusu Mafao mbalimabli yatolewayo na Shirika hilo ikiwemo Mango mpya kwa ajili ya Wakulima na Wachimbaji wadogo wa Madini.

Katika mpango huo, Wakulima sasa wanaweza kujiunga na NSSF na kufaidika na Mafao mbalimbali yanayotolewa na NSSF. Pia Wakulima wanaweza kufaidika na mikopo mbalimbali ikiwemo mikopo ya pembejeo na Vifaa.

Vilevile wakazi wa Mkoa wa Morogoro na wale kutoka Halmashauri mbalimbali Nchini wanaweza kupata elimu kuhusu uchangiaji wa Hiari, Kupitia Mpango huu.

Wote walio katika sekta isiyo rasmi, wafanyakazi, wafanyabiashara wanaweza kujiunga na NSSF na kufaidika na Huduma  mbalimbali kama vile Mafao ya Matibabu na Mikopo kupitia SACCOS.
 
Ofisa wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Marcel Amani (kulia), akimwelewesha mmoja wa washiriki katika mashindano ya SHIMISEMITA kuhusu Mafao ya muda mfupi yanayotolewa na NSSF yakiwemo mafao ya matibabu, mafao ya Uzazi pamoja na msaada wa mazishi kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro juzi. (Na Mpiga Picha Wetu)
Wachezaji wa Mpira wa Kikapu wakichuana vikali katika mashindano ya SHIMISEMITA yaliyodhaminiwa na NSSF katika viwanja vya Jamhuri Mkoani Morogoro. Tamasha hilo linahusisha michezo ya aina yote.
Ofisa wa NSSF  Ahmed Aly akimwandikisha katibu wa SHIMISEMITA, Salehe Lubawa kuwa mwanachama mpya wa NSSF kupitia mpango wa uchangiaji wa Hiari (Hiari Scheme).
Ofisa wa NSSF, Aisha Sango akitoa ufafanuzi kwa mmoja wa washiriki wa michezo ya SHIMISEMITA, kuhusu Mpango mpya kwa ajili ya Wakulima (Wakulima Scheme) katika viwanja vya Jamhuri Mkoani Morogoro.

No comments:

Post a Comment

Pages