HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

December 23, 2014

TTCL yatoa msaada kwa wagonjwa

Mkuu wa Huduma kwa Wateja wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Laibu Leonard(kushoto) akikabidhi msaada wa vyakula mbalimbali Muuguzi Mkuu wa Taasisi ya Saratani Ocean Road, Mary Haule kwa ajili ya kuwafariji wagonjwa waliolazwa katika hospitalini  hiyo. Wa pili kushoto ni Meneja Mauzo, Benjamin Bizere. (Picha na Francis Dande)
Mkuu wa Huduma kwa Wateja wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Laibu Leonard (kushoto) akikabidhi msaada wa vyakula mbalimbali Muuguzi Mkuu wa Taasisi ya Saratani Ocean Road, Mary Haule kwa ajili ya kuwafariji wagonjwa waliolazwa hospitalini hapo.Wa pili kushoto ni Meneja Mauzo, Benjamin Bizere.
Muuguzi Mkuu wa Taasisi ya Saratani Ocean Road, Mary Haule akipokea msaada wa vitu mbalimbali vilivyotolewa kwa ajili ya wagonjwa wa waliolazwa katika Taasisi ya Saratani jijini Dar es Salaam kulia ni Meneja Mauzo, Benjamin Bizere.
Mkuu wa Huduma kwa Wateja wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Laibu Leonardakizungumza na waandishi wa habari.
Muuguzi Mkuu wa Taasisi ya Saratani Ocean Road, Mary Haule  akizungumza na waandishi wa habari.

XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX

WAGONJWA wa saratani waliolazwa katika hospitali ya Ocean Road wamepata msaada wa vyakula kwa ajili ya sherehekea Siku Kuu ya Krismas inayotarajiwa kuadhimishwa kesho.

Msaada huo wenye tamani ya sh milioni tatu umetolewa na Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL).

Akizungumza na wandishi wa habari wakati akikabidhi msaada huo jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Huduma kwa Wateja, Laibu Leonard, alisema msaada huo ni sehemu ya kurudisha faida kwa wateja wao.

Alitaja msaada huo kuwa ni unga, majisafi, mchele na mwingine ambao utaweza kuwafariji, hususan katika kipindi hiki cha siku kuu hiyo.

“Hawa ni teja wetu ambao pia tunatarajia kuwafikishia huduma za afya mtaandao katika kipindi cha miezi mitatu, ambao utawasidia madaktari nchini kuwasiliana na wale wanje katika majidiliano yanayohusu matibabu  ya wagojwa bila kupata gharama za kuwapeleka nje,”alisema Laibu.

Naye Muguuzi Mkuu wa Hospitali hiyo, Mary Haule, alisema msaada huo umekuja katika kipindi muwafaka kwani kuna wagonjwa ambao wako hospitalini hapo hawana ndugu, utawasaidia.

“Tunaishuru TTCL kwa Msaada huu, tunawaomba wadau wengine watakaoguswa waige mfano huu,”alisema Mary.

No comments:

Post a Comment

Pages