HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

February 08, 2015

Jamii yatakiwa kutoa kipaumbele kwa vijana wakati wa mipangilio ya bajeti zao

Mke wa Rais wa Shirikisho la Jamhuri ya Ujerumani Bibi. Daniela Schadt  (mwenye nguo nyekundu) akisalimiana na Mkurugenzi wa DSW Tanzania Bw. Peter Owaga mara baada ya kuwasili katika ofisi za Shirika hilo zilizopo Tengeru jijini Arusha alipoenda kuzindua mradi wa BEYOND 2015 hivi karibuni.

Mke wa Rais wa Shirikisho la Jamhuri ya Ujerumani Bibi. Daniela Schadt  (mwenye nguo nyekundu) akisikiliza maelezo mafupi kuhusu Shirika lisilo la Kiserikali la DSW Tanzania kutoka kwa Mkurugenzi wa shirika hilo Bw. Peter Owaga mara baada ya kuwasili katika ofisi za Shirika hilo zilizopo Tengeru jijini Arusha juzi.Wa mwisho kushoto ni Mkuwa Wialaya ya Arumeru Mhe. Nyirembe Munasa

Mkurugenzi wa DSW Tanzania Bw. Peter Owaga akizungumza jambo wakati wa hafla ya uzinduzi wa mradi wa BEYOND 2015 juzi jijini Arusha. Kutoka kushoto ni Mke wa Rais wa Shirikisho la Ujerumani Bibi. Daniela Schadt, Mke wa Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania Bibi. Wenday Marshall – Kochanke na Mratibu wa Programu za Vijana kutoka Wizara ya Afya, na Ustawi wa Jamii Dkt. Elizabeth Mapella. BEYOND 2015 ni mradi uliolenga kuongeza hamasa na ushawishi kwa wadau wa maendeleo kutoa kipaumbele kwa vijana husasni katika Elimu, Afya ya uzazi na Ajira.


Baadhi ya washiriki wa hafla ya uzinduzi wa mradi wa BEYOND 2015 wakimsikiliza Mkurugenzi wa DSW Tanzania Bw. Peter Owaga (hayupo pichani).

Mke wa Rais wa Shirikisho la Jamhuri ya Ujerumani Bibi. Daniela Schadt(mwenye nguo nyekundu) akisikiliza maelezo kuhusu mradi wa BEYOND 2015 kutoka kwa Mratibu wa mradi huo Bi. Esther Mwanjesa (kushoto) kabla ya kuzindua rasmi mradi huo juzi jijini Arusha. Wa kwanza kulia ni Mkurugenzi wa DSW Tanzania Bw. Peter Owaga na kushoto kwa Mke wa Rais wa Ujerumani ni Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe. Nyirembe Munasa.

Mke wa Rais wa Shirikisho la Jamhuri ya Ujerumani Bibi. Daniela Schadt akifuarahi mara baada ya kukata utepe na kuzindua rasmi mradi wa BEYOND 2015, juzi jijini Arusha.Kushoto kwake ni Mkurugenzi wa DSW Tanzania ambao ndiyo watekelezaji wa mradi huu Bw. Peter Owaga. Wengine ni Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe. Nyirembe Munasa (nyuma ya Mke wa Rais wa Ujerumani) na Mratibu wa Mradi huo Bi. Ester Mwanjesa aliyeshika kitabu.

Mke wa Rais wa Shirikisho la Jamhuri ya Ujerumani Bibi. Daniela Schadt akiteta jambo na Mkurugenzia wa DSW Tanzania(katikati) pamoja na Mratibu wa Mradi wa BEYOND 2015 Bi. Esther Mwanjesa mara baada ya kuzindua mradi huo juzi jijini Arusha.

Mke wa Rais wa Shirikisho la Jamhuri ya Ujerumani Bibi. Daniela Schadt akipokea zawadi ya Kimasai kutoka kwa Mwanamke mjasiriamali Bibi.Salome Samwel wakati alipotembelea maonyesho ya biaadha zao katika hafla ya uzinduzi wa mradi wa mradi wa BEYOND 2015, juzi jijini Arusha.

Mke wa Rais wa Shirikisho la Jamhuri ya Ujerumani Bibi. Daniela Schadt akivaa heleni alizopewa kama zawadi kutoka kwa Mwanamke wa mjasiriamali Bibi.Salome Samwel wakati alipotembelea maonyesho ya biadhaa zao yaliyokuwa katika hafla ya uzinduzi wa mradi wa BEYOND 2015, juzi jijini Arusha.

Mke wa Rais wa Shirikisho la Jamhuri ya Ujerumani Bibi. Daniela Schadt  na Mwanamke mjasiriamali mwenye asili ya Kimasai Bibi.Salome Samwel wakiwa katika nyuso za furaha juzi jijini Arusha wakati wa hafla ya uzinduzi wa mradi wa BEYOND 2015 unaoratibiwa na kutekelezwa na DSW Tanzania.
Mke wa Rais wa Shirikisho la Jamhuri ya Ujerumani Bibi. Daniela Schadt akiangalia  zawadi ya michoro ya kitamaduni aliyopewa na Shirika la DSW Tanzania wakati wa hafla uzinduzi wa  mradi wa BEYOND 2015 juzi jijini Arusha. Aliyemshikia zawadihiyo ni Mkurugenzi wa DSW Tanzania Bw. Peter Owaga na Afisa Miradi wa  DSW Tanzania Bi. Diana Shuma (mwenye shati jeupe).

PIX8: : Mke wa Rais wa Shirikisho la Jamhuri ya Ujerumani Bibi. Daniela Schadt (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Shirika la DSW Tanzania wakati wa hafla ya uzinduzi wa mradi wa mradi wa BEYOND 2015, juzi jijini Arusha.Waliokaa kutoka kushoto ni Mke wa Balozi wa Ujerumani hapa nchini Bibi. Wenday Marshall – Kochanke, Mkuu wa Wialaya ya Arumeru Mhe. Nyirembe Munasa, Mkurugenzi wa DSW Tanzania Bw. Peter Owaga na Mratibu wa Programu za Vijana kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Elizabeth Mapella. Na Mpiga Picha Wetu, Arusha

No comments:

Post a Comment

Pages