HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

February 12, 2015

Red Arrows FC kujifua Tanzania

TIMU ya Red Arrows FC ya Zambia, inatarajiwa kuwasili jijini Dar es salaam, Tanzania Jumatatu ya wiki ijayo, kwa ajili ya kuweka kambi ya mafunzo ya wiki moja kujindaa na msimu mpya wa Ligi Kuu ya Zambia 2015.

Uongozi wa klabu hiyo chini ya Mwenyekiti wake Kanali Nolacso Chilando, ulitua jana Makao Makuu ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), sambamba na Ofisa Habari wa Red Arrow, Luteni Kanali, Melody Siisii.

Kwa mujibu wa taarifa ya TFF kwa vyombo vya habari, Chilando na Siisii, waliambatana na Alex Chila, ambaye ni Ofisa Ubalozi wa Zambia nchini Tanzania kujitambulisha uwepo wao nchini kuelekea wiki moja ya maandalizi.

Wakiongea na Katibu Mkuu wa TFF, Selestine Mweisgwa, viongozi wa timu hiyo wamesema maandalizi ya kambi yameshakamilika na kikubwa walikua wanaiomba TFF kutambua uwepo wao na kuwasaidia kupata viwanja vya kufanyia mazoezi.

Naye Katibu Mkuu wa TFF, Mwesigwa alisema wameyapokea maombi hayo ya Red Arrows FC na kuwakaribisha nchini kwa ajili ya kambi yao na kusema ujio wao utafungua milango kwa vilabu vingine pia kuja kuweka kambi nchini. Red Arrows inayomilikiwa na Jeshi la Anga la Zambia, ikiwa nchini kwa mafunzo, inatarajia kucheza mchezo mmoja wa kirafiki na imeliomba TFF kuwatafutia timu moja ya kucheza nayo.

No comments:

Post a Comment

Pages