HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

April 27, 2015

Mchungaji; Nitaacha Madhabahu, tumpate Rais mwenye Sifa.

MCHUNGAJI, Alphonce Temba, wa Kanisa la Penuel Healing Ministry Dar es Salaam, amesema ataacha Madhabahu kuwahubiri Waumini, na badala yake atakwenda kushirikiana na Wanasiasa kuwaelimisha Wananchi ili Tanzania impate Rais mwenye Sifa, na atakayetatua Ajali zinazomaliza Maisha ya Watu.

Akizungumza ITV katika Kipindi cha Kumekucha asubuhi Aprili 27, mwaka huu, Temba alisema, Tatizo kubwa la ajali  zinazomaliza Watanzania nchini zinatokana na Uzembe wa Viongozi, Ubovu na Uchache wa Miundo mbinu ya barabara zetu na kudai, ataacha Madhabahu na kuungana na Wanasiasa, kuhakikisha anapatikana Rais mwenye Sifa, atakayezua ajali.

Hata hivyo Mchungaji Temba, alimshambulia Waziri wa Ujenzi John Pombe Magufuli akisema, ajali nyingi zimetokea na watu wengi wamekufa kwa kumwaga damu, lakini hajasikika akitoa tamko lolote na akamtuhumu kuwa, kuna Sheli za Mafuta na Gereji zimejengwa barabarani (mfano Kibaha), lakini hachukui hatua.

Temba alidai, “Nadhani Magufuli amechoka na anatakiwa kusaidiwa na Vijana wengine wasomi, ambao wana uwezo mkubwa wa Teknologia mpya lakini wanakosa kazi. Ingawa wanasiasa wanasema Viongozi wa dini tusiwaingilie,  tupo kwa ajili ya kuwakemea.

“Katika nchi za wenzetu kuna barabara sita na magari yanakwenda mwendo wa kasi, lakini hakuna ajali! Kwetu kuna ajali kwa sababu barabara ni moja, Malori yanaingia mjini badala ya kuishia nje ya mji ili kupunguza msongamano”.

Mbali ya kumshambulia Waziri Magufuli, pia Temba aliwaone Askari wa Usalama barabarani (Traffic) na kuwavaa Watendaji wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROAD) akidai, Polisi sasa hivi wamefanywa kama TANROAD, walichobakiza ni kujenga kwa sababu, siku hizi kila kitu ‘Traffic’.

Temba alishauri, Safari za Mabasi kusafiri usiku, zierejeshwe kwa sababu zitapunguza msongamano wa Magari, na kudai, Viongozi wa dini na Wananchi waheshimiwe, na kwamba, sasa kazi yetu iwe ni kuwafukuza wafanyakazi wazembe, ili wasomi wasio na kazi wachukue nafasi zao maendeleo ya nchi yaende.

No comments:

Post a Comment

Pages