HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

July 13, 2015

Msama awapiga tafu Kwaya ya Mt. Cesilia

Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion, Alex Msama akiwa amenyanua juu DVD, kama ishara ya uzinduzi wa albamu ya ‘Jipange Dunia’  ya Kwaya ya Mt. Cecilia mjini Dodoma juzi. (Picha na Danson Kaijage)

NA MWANDISHI WETU, DODOMA

MKURUGENZI wa Kampuni ya Msama Promotions ya jijini Dar es Salaam, Alex Msama, mwishoni mwa wiki alikuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa DVD za albamu ya ‘Jipange Dunia’ ya Kwaya ya Mt. Cesilia ya Parokia ya Mt. Maria Imaculata.

Akizungumza katika uzinduzi huo uliofanyika katika kanisa hilo lililopo eneo la Bihawana, nje kidogo ya mji wa Dodoma, Msama mwasisi wa matamasha ya muziki wa injili nchini, alitoa wito kwa wenye kipaji kuitambua talanta yao.

Msama alisema kazi ya uimbaji ni wito na ni huduma ambayo inatolewa na waimbaji kwa ajili kusaidia roho za watu zisipotee kwa kuishi maisha ya mema ya kumtumaini na kumpendeza Mungu kama vitabu vitakatifu vinavyoagiza.

Aidha, Msama alikubali ombi la Kwaya hiyo kuwa mlezi akisemo hiyo ni heshima kubwa kwake kwani imeonesha ni kwa jinsi gani walivyomthamini kuanzia suala la kumpa heshima ya kuwa mgeni rasmi.

‘’Nimekubali kuwa mlezi wa kwaya hii,ninashukuru kwa kunidhamini na kunialika kuwa mgeni rasmi,mimi nipo Dar es salaam lakini mmenialika mimi na kuwaacha watu wengi hapa Dodoma,’’ alisema Msama na kuongeza:

‘’Nimekuja kusaidia kwa sababu kutoa sio utajiri wala sina mali nyingi, ila namtumikia Mungu kwa njia hii kwa kuwa ninajua nilipotoka,’’ alisema Msama mmoja wa watu wenye moyo wa kusaidia makundi mbalimbali katika jamii kama yatima, walemavu na wajane.

Awali, akisoma risala, Exaveli Sudai alisema kwaya hiyo inakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo kukosekana kwa fedha pamoja na vitendea kazi vya uimbaji na kuomba sapoti zaidi ili waweze kufikia malengo ya kuhubiri injili ya Mungu.

Mbali ya Msama kutoa kiasi hicho, pia aliendesha harambee iliyozaa matunda ya kupatikana sh. milioni 3.4  na ahadi sh. mil 1.3, hivyo fedha taslimu na ahadi kufikia jumla ya shilingi mil 4.7.

No comments:

Post a Comment

Pages