HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

August 16, 2015

MSAMA KUOMBEA UCHAGUZI MKUU

  Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotions, Alex Msama akifafanua jambo wakati wa mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, kuhusu tamasha kubwa la kuiombea amani nchi litakalofanyika Okroba 4. (Picha na Francis Dande)


NA FRANCIS DANDE

KAMPUNI ya Msama Promotions imeandaa Tamasha kubwa la kihistoria ambalo halijawahi kufanyika nchini la kuiombea Tanzania inayoelekea katika uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotions Alex Msama Tamasha hilo litafanyika Oktoba 4, jijini Dar es Salaam.

Msama alisema kutokana na uzito na heshima ya tamasha hilo, linatarajia kushirikisha waimbaji mbalimbali wa nyimbo za injili wa ndani na nje ya nchi ambao wanaotamba katika tasnia ya muziki huo.

Alisema japo ni mara ya kwanza kwa kampuni yake kuandaa tamasha kama hilo katika historia ya uchaguzi nchini, anaamini kwa vile amani ni kitu muhimu katiika uchaguzi, wengi watamuunga mkono.
Msama alisema anaamini wengi watajitokeza kuungana pamoja na viongozi wa kitaifa na kada mbalimbali kuuombea uchaguzi huo ambao ni njia ya kidemokrasia ya kupata viongozi kwa ngazi ya urais, ubunge na udiwani.

“Watanzania wajiandae kuiombea amani Tanzania kupitia muziki wa Injili hasa waimbaji mbalimbali wa kutoka nje ya Tanzania watashiriki katika tukio hilo ambalo bado tuko katika mchakato wa mahali tutakapofanyia,” alisema Msama na kuongeza:

“Tamasha hilo kubwa kimaudhui linakaribia Tamasha kubwa la Pasaka ambalo hufanyika kila mwaka tangu mwaka 2000,” alisema Msama aliyechangia kwa kiasi kikubwa kukua kwa muziki wa injili.

Aidha Msama alisema baada ya tamasha hilo kufanyika jijini Dar es Salaam, watahamishia maombi hayo katika majiji mengine manne kwa lengo hilo la kuombea amani na utulivu uchaguzi Mkuu.   

Alitaja nchi watakazotoka waimbaji watakaosindikiza maombi hayo ni
Afrika Kusini, Rwanda, Kenya, Uganda, Zambia, Burundi na DR Congo.

No comments:

Post a Comment

Pages