Muonekano
wa Jengo la Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi ambalo limefunguliwa rasmi na Rais
Kikwete mjini Dodoma.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete (katikati) kwa
pamoja na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Prof. Mussa
Assad (kulia) na Waziri wa Fedha Mhe. Saada Mkuya (kushoto) wakikata utepe
kuashiria ufunguzi rasmi wa Jengo la Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi, mkoani Dodoma.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete (katikati waliokaa)
akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi waandamizi wa Ofisi ya Taifa
ya Ukaguzi mara baada ya kulifungua rasmi Jengo la Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi,
mkoani Dodoma.
Saidi Ahmed Mkabakuli
Mheshimiwa
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, leo,
tarehe 15 Oktoba, 2015, amelifungua rasmi jengo la Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi
mkoani Dodoma.
Akizungumza
wakati wa ufunguzi huo, Rais Kikwete ameipongeza Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi kwa
kujenga jengo zuri linaloakisi sifa na heshima ya utendaji wa Ofisi hiyo.
Kwa
upande wake CAG, aliishukuru Serikali ya Awamu ya Nne kwa kuiwezesha ofisi yake
na kuongeza uhuru wa ofisi hiyo kwa kuwawezesha kujenga majengo katika mikoa ya
Singida, Morogoro na Kilimanjaro.
Ufunguzi
huo ulishuhudiwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Prof.
Mussa Assad, baadhi ya viongozi waandamizi na watumishi wa Ofisi ya Taifa ya
Ukaguzi kutoka Makao Makuu na Dodoma. Kwa upande wa Wizara ya Fedha
walioshuhudia ni Waziri wa Fedha, Bibi Saada Mkuya na Katibu Mkuu wake, Dkt.
Servacius Likwelile.
Jengo
hili limekusudiwa kuwa makao makuu ya Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi.




No comments:
Post a Comment