Mbunge mteule katika Jimbo la Manonga wilaya ya Igunga mkoani Tabora , Seif Khamis Gulamali (CCM) akiwashukuru wananchi wa Kata ya Ndebezi katika jimbo hilo kwa kumpa kura za kishindo, madiwani na Dkt. John Magufuli aliyekuwa anawania kiti cha urais.
Wananchi wa Kata ya Ntobo wakishangilia kwa furaha mara baada ya Mbunge mteule katika Jimbo la Manonga wilaya ya Igunga mkoani Tabora , Seif Khamis Gulamali (CCM) alipowasili eneo hilo kwa kutoa shukrani kwa wananchi hao kwa kumchagua katika uchaguzi uliofanyika wiki iliyopita.
Akizungumza na wakazi wa Kata ya Choma, Mbunge mteule katika Jimbo la Manonga wilaya ya Igunga mkoani Tabora , Seif Khamis Gulamali (CCM) alisema ushindi wa kura 31,485 sawa na asilimia 67. 65 aliopewa na wana Manonga dhidi ya Ally Nguzo wa Chadema aliyepata kura 14,420 sawa na asilimia 30.96. Amesema atahakikisha anawapa wananchi hao ushirikiano, usimamizi na utatuzi wa changamoto mbalimbali zinazowakalibi.“
Mke wa Mbunge Mteule Bi Sarah Abdallah akitoa shukrani kwa wananchi wa kata ya Choma kwa kazi nzuri waliyoifanya.
Mbunge mteule Jimbo la Manonga Wilaya ya Igunga mkoani
Tabora , Seif Khamis Gulamali (CCM) akiwapungia mkono wananchi wa
kata ya Mwashiku wakati wa mkutano wa kuwashukuru baada ya
kuchaguliwa kuwa mbunge wa jimbo hilo.
Hakika ilikuwa ni siku ya furaha kwa wakazi wa jimbo la Manonga
No comments:
Post a Comment