HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

November 13, 2015

MTOTO WA MWAKA MMOJA AFARIKI DUNIA BAADA YA KUTUMBUKIA KISIMANI MBEYA

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Ahmed Msangi.


Na EmanuelMadafa, Mbeya 

Mtoto mwenye umri wa mwaka mmoja na miezi saba  Promis Dank mkazi wa bwawani wilaya ya chunya alifariki dunia njiani akiwa anapelekwa hospitali baada ya kutumbukia kisimani.

Tukio hilo limetokea Novemba  112  majira ya saa 12 asubuhi huko kitongoji cha railway,  kata ya bwawani, wilaya ya chunya, mkoa wa mbeya. 

Inadaiwa kuwa, mtoto huyo baada ya kutumbukia kwenye kisima hicho ambacho kilikuwa wazi, aliokolewa akiwa hai lakini alifariki dunia akiwa njiani kuelekea hospitali teule ya mwambani kwa matibabu.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya  Ahmed z. Msangi ametoa wito kwa wazazi na walezi kuwa makini hasa kwa kuweka uangalizi wa kutosha kwa watoto wadogo ili kuepuka madhara yanayoweza kuepukika. 

Aidha anatoa wito kwa jamii kufunika visima vilivyowazi, kufukia mashimo yenye maji kwani ni hatari kwa watoto wadogo hasa katika msimu huu wa mvua za vuli.

(JAMIIMOJABLOG MBEYA )

No comments:

Post a Comment

Pages