Na Mwandishi Wetu
MBUNGE
wa Muheza, Balozi Adadi Rajabu (pichani), anatarajia kukutana na wa Wakazi wa wilaya hiyo,
wanaoishi jijini Dar
es Salaam kesho, kwa ajili ya kuzungumzia mipango ya utekelezaji wa
maendeleo katika jimbo hilo.
Akizungumza
na wandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mratibu wa Mkutano huo,
Clement Mang’enya, alisema wilaya ya muheza hivi sasa imejipanga kuwasogezea
maendeleo karibu wakazi wote, hata hivyo, yote hayo yatafanikiwa iwapo watakuwa
msitari wa mbele katika kutoa
ushirikiano.
“Mkutano
huo, utafanyika katika kijiji cha Makumbusho Kijitonyama jijini, kuanzaia saa 3
asubuhi kwa hiyo, ni fursa nzuri kwa Wanamuheza kujitokeza kwa wingi ili kuja
kuwa sehemu ya watakaotoa mawazo ya nini kifanyike katika kipindi hiki cha
miaka mitano ya Balozi Adadi,”alisema Mang’enya.
Alisema,
katika mkutano huo mambo mabalimbali yatajadiliwa lakini kubwa litakalochuku
nafasi kubwa litakuwa la kuzipatia madawati shule zote za wailaya hiyo, ili
kuwaondolea adha ya kukaa chini baadhi ya wanafunzi.
“Hivi
sasa tumejipanga katika kuondoa baadhi ya kero ambazo nyingine ni za miaka
mingi kwa hiyo kupanga ni kuchagua hivyo basi katika miaka hii mitano
tumechagua kujiletea maendeleo ambayo tumeyahitaji kwa miaka mingi,”alisema
Mang’nya.
Mang’enya,
alisema mkutano huo, pia utakuwa na agenda ya uhuishaji wa Mfuko wa Maendeleo
wa Muheza (MTDF), lengo likiwa ni pamoja na kupata viongozi na wajumbe ambao
watausimamia kwa ufanisi mfuko huo ukilinganisha na sasa.
Aidha,
Mang’enya alitoa wito kwa wakazi wanaoishi katika mikoa mingine nchini kuandaa
mikutano kama hiyo, yenye lengo la kusaidia jimbo lao kimaendeleo ambayo
yataijengea heshima wilaya yao.
No comments:
Post a Comment