Na Talib Ussi, Zanzibar
Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) imesema uchaguzi wa marejeo uko
pale pale licha ya baadhi ya waangalizi wa kimataifa kusema hawatoshiriki
uchaguzi huo.
Hayo yalielezwa na
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Mohammed Aboud Muhammed
alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari huko Ofisini kwa Vuga Mjini hapa.
Alisema wao hawataacha
kufanya shuhuli yao eti kwa sababu hakuja mtu Fulani kushuhudia.
“Sisi hatujawahi kutuma
watu kwenda kuingilia uchaguzi wa Marekeni kwa hiyo na sisi hatuoni haja
tusiendelee na shuhuli yetu” alisema Mohammed.
Alisema wanavyoamini
uchaguzi umefutwa na Tume ya Uchaguzi iliyohuru kwa hiyo hawana budi kukubali
maamuzi ya ZEC.
“Tume yetu ipo kikatiba
na haingiliwi kwa mujibu wa katiba lazima tuheshimu maamuzi yake” alieleza
Mohammed.
Sambamba na hilo waziri
huyo alisema SmZ itahakikisha amani na utulivu ulio mkubwa unakuwepo kwenye uchaguzi
huo.
Aliwataka wananchi
kujitokeza kwa wingi bila woga kwenda kufanya maamuzi yao kwa kuchagua viongozi
wanao wataka.
“Maamuzi ya wananchi
yataheshimiwa kwa mujibu wa sheria ziliopo” alisema Mohammed.
Siku za hivi karibuni
Jumuiya ya Ulaya na Marekani walitangaza wazi kwamba hawatashiriki uchaguzi huo
wa marejeo kwa kile walichosema kwamba ni batili.
Ama kwa upande wa JWTZ
na Vikosi vya SMZ kufanya mazoezi na kutembea na vifaru mitaani kipindi hiki
cha kuelekea kwenye uchaguzi huo, alisema hayo ni mazoezi yao ya kawaida
kuwataka wananchi kuondoa ghofu.
Alisema mara nyingi
inapofika wakati kama huu JWTZ na Vikosi vya SMZ hufanya mazoezi yao na kuambatana
na matembezi ya maeneo tofauti lakini mwaka huu yamesadifiana na uchaguzi wa
marejeo.
Hivi sasa JWTZ pamoja
na vokosi vya SMZ vinapita mabarabarani vikiwa na magari maji kuwasha na vifaru
katika maeneo yote ya Zanzibar.
No comments:
Post a Comment