Na Talib Ussi, Zanzibar
Wananchi wa Zanzibar wametakiwa
kuchukua tahadhari kutokana kuibuka upya ugonjwa wa Kipindupindu baada ya mvua
kuza kunyesha ndani ya siku mbili.
Akitoa tamko hilo
Daktari dhamana Unguja Fadhil Mohammed alisema kwamba wagonjwa 33 wamelzwa
katika kambi maalum za wagonjwa hao zilioko Chumbuni Wilaya Mjini 31,
Ukongongoroni Wilaya ya kati mmoja na Fujoni Wilaya ya kati mmoj kuazia Jumanne.
“Maradhi ya
kipindupindu yapo wananchi mnatakiwa kuchukua tahadhari kubwa kutokana kasi ya
ugonjwa huu” alisema Mohammed.
Alisema sababu ya
maradhi hayo ya mripuko ni kutona kuenea kwa uchafu katika mitaa mingi ya Zanzibar
jambo ambalo linaathiri wanachi sasa.
Alisema tokea Septemba
mwaka jana wagonjwa 1974 wametibiwa na kati yao 22 walifariki kutokana na
maradhi hayo.
Ali Juma ambaye ni
mkurugenzi wa maafa Zanzibar alisema utupaji wa vitu ovyo katika masalio ya
maji imepeleke mvua zinaponyesha kuwepo kwa ucahfu mwingi.
“Watu wetu wamezoea
kutpa ovyo ovyo manepi na Penpasi pasina kuzingatia kwamba lile linaweza
kuwaathiri baadae” alisema Juma.
Alisema dini zoote
zinahimiza usafi kwa hiyo aliwataka wananchi kuweka usafi katika maeneo yao na
kuwa waangalifu na watoto wasichezee vitu vilivyooza.
Alifahamisha kuwa
changamoto kubwa wanayoipata katika kupambana na maradhi hayo ni kuwepo katika
maeneo tofauti visiwani humu.
“Tuweni makini zaidi na
watoto wetu kwani wao huchezea kila kitu bila ya kujua kwamba wanaweza
kuathirika” alieleza Juma.
Kutokana na suala hilo
alivitaka vyombo vya habari kuwaelimisha wananchi katika kupambana maradhi
hayo.
No comments:
Post a Comment