Na
Mwandishi Wetu, Zanzibar
WAJUMBE wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar wameitaka Ikulu kuhakikisha ahadi za rais zinatekelezwa kwa wakati muafaka ili kufikia malengo yaliykusudiwa.
Akizungumza
wakati akichagia hotuba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi aliyoitoa wakati akizindua Baraza la Tisa, Mwakilishi wa Jimbo
la Uzini, Muhammed Raza Dharams, alisema mara nyingi rais anapokwenda
katika kazi za kuzindua skuli au hospitali,
gharama za mapambo ni zaidi Sh. Milioni 20.
“Lakini
rais akitoa hadi ya milioni mbili tu basi, inawezekana kuchukua miaka yote
mitano haijatimizwa ahadi hiyo,” alisema Raza.
Alisema
ni vema watendaji wakawajibika ipasavyo na kufanya majukumu yao kwa mujibu wa
maelekezo waliyopewa ili maendeleo ya nchi yaweze kuonekana.
“Mimi
nina ushahidi, akienda sehemu rais, basi hutafutwa tajiri akaambiwa toa milioni
20 haraka haraka, lakini subiri hiyo ahadi, hapo ndiyo balaa,” alieleza Raza.
Kwa
upande wake Mwakilishi wa kuteuliwa na Rais, Hamad Rashid Muhammed, aliwaomba
viongozi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwenda na wakati na kuacha
kulewa mazoea.
“Viongozi
wetu hawana uwajibikaji ambao unatakiwa hasa katika kipindi hiki kigumu
tunachoelekea” alieleza Muhammed.
Alisema
kama watajitahidi kukusanya mapato na yakatumiwa
kwa kinachokusudiwa, basi hakutakuwa na haja ya kutegemea wahisani ambao wanadai kuzuia misaada yao.
kwa kinachokusudiwa, basi hakutakuwa na haja ya kutegemea wahisani ambao wanadai kuzuia misaada yao.
“Tufanyeni kazi kwa manufaa ya nchi yetu na si kwa matakwa ya mtu binafsi ili maendeleo yetu yaonekane,” alieleza Muhammed.
Aidha,
kwa upande wa mwakilishi wa Jimbo la Kijito Upele, Ali Suleiman Ali, alisema
kama viongozi wa SMZ watafanya kazi kwa nia njema, maendeleo yanaweza
kuonekana.
“Tumeshasikia
Marekani na wenzake wameshaaza kuzuia misaada yao kwetu, sasa tuchangamkeni na
watakaochaguliwa mawaziri washuke hata mabondeni,” alisema Ali wakati
akichangia hotuba ya Rais wa Zanzibar.
Baraza
hilo la wawakilishi linaloendelea hapa litegemewa kuahirishwa Ijumaa ijayo
baada ya wajumbe wote kupata fursa ya kuchangia hotuba hiyo.
No comments:
Post a Comment