HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

May 16, 2016

Mama Samia aifagilia kampuni ya Superdoll

NA MWANDISHI WETU

MAKAMU wa Rais, Samia Suluhu Hassan ameitaka kampuni maarufu ya matairi nchini ya Superdoll kuendeleza uwekezaji katika maeneo ya ukanda wa kilimo kwa ajili ya kuinua sekta hiyo muhimu kwa maendeleo ya nchi na watu wake.

Mama Samia aliyasema hayo mwishoni mwa wiki katika hafla ya uzinduzi wa kituo cha huduma za magari cha kisasa cha Superdoll na matairi ya BF Goodrich KO2, jijini Arusha ambayo yatakuwa ufumbuzi wa tatizo sugu la matairi yasiyo na kiwango hivyo kushindwa kuhimili mazingira ya barabara za mbugani.

Kupitia hafla hiyo ya uzinduzi iliyoshuhudiwa pia na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Daud Felix Ntibenda, Mama Samia alimpongeza Mkurugenzi wa kampuni ya Superdoll, Seif A. Seif kwa kumwalika katika hafla hiyo iliyompa fursa ya kusalimiana na wadau wa sekta binafsi.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa kampuni hiyo (Seif), mbali ya kumshukuru Mama Samia kukubali ombi la kumtaka awe mgeni rasmi katika uzinduzi wa matairi bora ya BF Goodrich K02, alisema matairi hayo yatasaidia sekta ya utalii kwa mkoa wa Arusha.

Alisema Seperdoll ambayo ni wasambazaji wa matairi namba moja kwa ubora duniani ya Michelin, ni fahari kwao kuwekeza katika ujenzi wa kituo cha kisasa cha BF Goodrich kwa kuwa na mashine zenye ubora wa hali ya juu.

“Uwekezaji huu umelenga zaidi kwenye kuhakikisha tunakuza wiwango vya usalama barabarani kwa wananchi na kwa watalii wanaokuja nchini. Kwa njia hii tutaweza kukuza kukuza zaidi soko letu la
sekta ya utalii na kuongeza pato la taifa,” alisema Seif.

Seif alitoa wito kwa wadau mbalimbali wa sekta ya utalii wa jijini Arusha kukitumia kituo hicho kikamilifu huku akiahidi kuwa huduma itakuwa bora chini ya mawakala wao waliopo jijini Arusha
na Moshi, Mkoani Kilimanjaro.

                                              

No comments:

Post a Comment

Pages