Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili ya Shirikisho la Soka
Tanzania (TFF), Wakili Wilson Ogunde akisoma maamuzi ya kamati hiyo iliyoketi
jijini Dar es Salaam kuhusu shauri la msemaji wa Yanga, Jerry Muro ambapo
kamati hiyo imetoa hukumu ya kifungo cha mwaka mmoja kutojihusisha na masuala
ya soka. (Picha na Francis Dande)
KAMATI ya Maadili ya Shirikisho la Soka Tanzania TFF, chini ya
Mwenyekiti wake Wakili Wilson Ogunde imemfundia Ofisa Habari wa Klabu ya Yanga
Jerry Muro kujiusisha na masuala ya soka kwa muda wa mwaka mmoja sambamba na
faini y ash mil 3 kutokana na maneno yake ya uchochezi.
Awali kamati hiyo iliyokutana Julai 2 mwaka huu, ilishindwa
kutoa uamuzi dhidi ya Muro kutokana na madai ya kukosa wito uliomuelekeza rasm
kuitwa na Kamati hiyo, huku kamati hiyo ikitaka Sekretariet ya TFF kumuita tena
katika kikao cha kilichofanyika Jijini Dar es Salaam.
Akizungumza wakati wa kutoa hukumu hiyo Ogunda
amesema, baada ya kupitia mashauri matatu yaliyowasilishwa juu ya kamati yake,
kamati iliyapitia na kutoa hukumu kwa kusikiliza upande mmoja wa mshitaki
kutokana na mshitakiwa kushindwa kufika katika kikao hicho.
Ogunda ametaja mashtaka hayo matatu yaliyofika mbele ya
kamati yake kuwa ni kushindwa kutekeleza maamuzi ya kamati ya nidhamu
iliyomtaka kulipa faini y ash mil 5 baada ya kupatikana na hatia Mei 5 mwaka
jana, hivyo kutokana na kushindwa kutekeleza agizo hilo la kamati husika licha
ya Mei 10 kukumbushwa na TFF kamati imejilidhisha na kumtia hatiani kwa kumfungia
mwaka mmojakuanzia Julai 7 mwaka huu.
Aidha Ogunda aliyeambatana na Wajumbe wake watatu wa kamati
hiyo akiwemo Makam wake Mwenyekiti Ebeneza Mshana alisema shitaka la pili
lillilomtia hatiani Muro ni kutoa lugha ya kashfa kwa kupotosha maamuzi
ya TFF Juni 25 mwaka huu alitoa taarifa katika moja ya redia akipinga maamuzi
TFF kusaini mkataba wa Azam TV kwa niaba ya CAF akidai TFF wanawahujumu ili
wasipate mapato katika mchezo wao na Tp Mazembe. Kamati ya Maadili kamati
imejiridhisha kuwa Muro hana hatia katika shitaka hilo la pili,,alisema.
Kuhusu Shitaka la tatu Ogunde alisema mnamo Juni 26 kupitia
moja ya redia Muro alikaliliwa akivunja ukaaji wa mashabiki Uwanjani akidai wa
Simba wanatakiwa kukaa juu ya paa kitendo ambacho kingepelekea vurugu wakati
TFF walikuwa washatoa muongozo juu ya kukaa Uwanjani hapo.
Ambalo limemkuta na hatia ya kufungiwa mwaka mmoja ambayo
adhabu yake inaanza Julai 7 mwaka huu na adhabu zote za kufungiwa zitaenda
sambamba kwa maana ya kutumikia adhabu mbili kwa kipindi kimoja
Wakati huo huo kuhusu Nasseb Mabrouk ametakiwa kuhakikisha
anarejesha kiasi cha sh 949,767 ndani ya siku 30 kwa TFF ambazo alishindwa
kuziwasilisha akiwa msimamizi wa kituo cha Soka Mwanza.



No comments:
Post a Comment