HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

July 12, 2016

MRADI WA USAID WA UIMARISHAJI WA MIFUMO YA SEKTA ZA UMMA MKOANI WAZINDULIWA LEO

 Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Meja Generali (Mstaafu), Salum Kijuu akizungumza wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Uimarishaji wa mifumo ya sekta za Umma (PS3) unaotekelzwa katika mikoa 13 ya Tanzania bara kwa ushirikiano wa baina ya  Shirika la Misaada la Kimataifa la Marekani (USAID) na Serikali ya Tanzania. Mradi huo utazihusisha Halmashauri 93 katika mikoa hiyo.
Mtaalam wa fedha wa mreadi wa PS3 ambaye ndie msimamizi wa uzinduzi huo Mkoani Kagera, Abdul Kitula akielezea maeneo mbalimbali ambayo mradi huo utahusika na kufanya kazi. 



Kitula alisema PS3 inalenga kuunda ushirikiano na Serikali ya Tanzania kwa ajili ya kuimarisha mifumo ya sekta za umma yakiwemo masuala ya utawala bora, rasilimali watu, fedha, utoaji wa taarifa, na tafiti tendaji.

Wakuu wa Wilaya za mkoa wa Kagera wakifuatilia uzinduzi huo.
Mratibu wa Mradi wa PS3 kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Bertha Swai akijibu na kutolea ufafanuzi baadhi ya maswali yaliyoulizwa na washiriki.
  Mtaalam wa masuala ya Rasilimali watu kutoka Taasisi ya Benjamin Mkapa (BMF), Remmy Moshi akiwasilisha mada.

No comments:

Post a Comment

Pages