HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

October 22, 2017

KAMATI MPYA YA UONGOZI YA BODI YA LIGI KUKUTA

Kamati mpya ya Uongozi ya Bodi ya Ligi Kuu (TPLB) inafanya kikao chake cha kwanza Alhamisi, Oktoba 26 mwaka huu jijini Dar es Salaam.

Moja ya ajenda katika kikao hicho ni kuteua Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi, na kamati nyingine mbalimbali.

TPLB ilifanya uchaguzi Jumapili, Oktoba 15 mwaka huu na kupata uongozi mpya chini ya Mwenyekiti wake Clement Sanga.

Viongozi wengine waliochanguliwa ni Shani Mlingo (Makamu Mwenyekiti) na wajumbe Hamisi Madaki, Ramadhani Mahano, Almasi Kasongo na Egdar Chibura.

Boniface Wambura
Ofisa Mtendaji Mkuu
Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB)

No comments:

Post a Comment

Pages