HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

November 05, 2017

LAPF YACHANGIA SHILINGI MILIONI TANO UJENZI WA OFIFI ZA WALIMU MKOA WA DAR ES SALAAM

001
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mh. Paul Makonda akipokea Msaada wa Fedha Taslimu Shilingi Milioni tano 5.000.000/= kutoka kwa Bw. James Mlowe Meneja Mawasiliano na Masoko Mfuko wa Pensheni wa LAPF kwa ajili ya Kununulia mifuko 500 ya Saruji katika kuchangia kampeni ya ujenzi wa Ofisi za Kisasa za walimu katika shule za Msingi na Sekondari Mko wa Dar es salaam.
Kampeni hiyo imeanzishwa na Mkuu wa mkoa wa Mh.Paul Makonda katika jijini la Dar es salaam, ambapo Ofisi zaidi ya 400 zitajengwa katika shule za jiji la Dar es salaam hivyo kuboresha utendaji kazi wa waalimu hao, Kalia anayeshuhudia tukio hilo ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ujenzi Kanali Charles Mbuge, Makabidhiano hayo yamefanyika mwishoni mwa wiki ofisini kwa Mkuu wa mkoa.
01
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mh. Paul Makonda akimsikiliza Bw. James Mlowe Meneja Mawasiliano na Masoko Mfuko wa Pensheni wa LAPF wakati akizungumza kabla ya kukabidhi msaada uliotolewa na LAPF kwa mkuu wa mkoa wa Dar es salaam kwa ajili ya ujenzi wa ofisi za walimu katika shule za sekondari na Msingi katika mkoa wa Dar es salaam.
2
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mh. Paul Makonda akizungumza katika makabidhiano hayo yaliyofanyika Ofisini kwake katikati ni Bw. James Mlowe Meneja Mawasiliano na Masoko Mfuko wa Pensheni wa LAPF na kulia ni Kanali Charles Mbuge Mwenyekiti wa Kamati ya Ujenzi.
3
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mh. Paul Makonda akisisitiza jambo wakati akizungumza katika makabidhiano hayo yaliyofanyika Ofisini kwake lulia ni Bw. James Mlowe Meneja Mawasiliano na Masoko Mfuko wa Pensheni wa LAPF.

No comments:

Post a Comment

Pages