HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

November 12, 2017

RC Wangabo awashauri wakulima kuanzisha mpango wa chakula mashuleni

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo.

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amewataka wakulima kushirikiana na uongozi wa shule za msingi na sekondari Mkoani Rukwa kuanzisha utaratibu wa kuwalisha wananfunzi wanapokuwa mashuleni.

Amesema kuwa anafahamu kwamba Mkoa wa Rukwa ni miongoni mwa mikoa sita inayotegemewa kwa uzalishaji wa chakula nchini lakini haina utaratibu wa kuwalisha wananfunzi wanapokuwa mashuleni jambo linaloshusha ufaulu kwa wananfunzi hao.

“Tangu nimefika katika Mkoa huu wazee wananiambia hapa Rukwa kuna chakula cha kutosha, utakula kuanzia asubuhi hadi kesho yake asubuhi, namna chakula kilivyokuwa kingi lakini Je, humo mashuleni mwetu wanafunzi wanapewa chakula?” Aliuliza.

Ameyasema hayo alipokuwa akiongea na wazazi, walimu na wanafunzi katika shule ya Msingi kipili kata ya kipili, Wilayani Nkasi katika ziara yake ya kwanza tangu kuteuliwa na rais Dk. John Pombe Magufuli kuwa Mkuu wa Mkoa huo na lengo ikiwa ni kutembelea na kukagua miradi mabalimbali ya wilaya hiyo pamoja na kujitambulisha kwa wananchi.  

Ameongeza kuwa wanafunzi wamekuwa wakitembea umbali mrefu kwenda shule huku matumbo yakiwa matupu na hatimae wanashindwa kuelewa wanachofundishwa darasani kwa kusikilizia njaa.

“Kuwa na chakula kingi haitakuwa na maana kama watoto wetu wanashinda njaa mashuleni.”

No comments:

Post a Comment

Pages