HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

March 24, 2018

SHULE YA MSINGI UWONDWE YAKABILIWA NA UPUNGUFU WA VYOO

WANAFUNZI 1622 wa Shule ya  Msingi Uwondwe Shehia ya Mtambwe Mkoa wa Kaskazini Pemba, wako hatarini kupata maradhi ya mripuko iwapo hatua za haraka hazitachukuliwa kutokana na kujisaidia Vichakani karibu na eneo la shule kufuatia upungufu wa vyoo.

Taarifa hiyo ilitolewa na Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Khadija Said Khalfan mbele ya mkuu wa Mkoa huo alipofanya ziara ya khafla kujione mwenyewee tatizo hilo.

 “Mh; kiukweli shule yetu ina vyoo vitatu na idadi ya wanafunzi kama hivyo na kipindi hichi mvua ndio tukasema kuwa tumo katika hatari ya maradhi mengi ikiwemo ya mripuko kama hatua za haraka hazikuchukuliwa” alieleza Mwalimu Mkuu.

Alifahamisha kuwa watoto wengi wanao tumia shule hiyo ni wadogo ambao wanaposhikwa na haja kubwa na ndogo hukimbilia vichaka ili kuondoa shida yao kutokana hivyo vyo kuwa vibovu ambavyo alieleza kuwa vimejengwa tangu kabla ya Mapinduzi.

Naye Mkuu wa mkoa wa Kaskazini Pemba  Omar Khamis Othman ambaye ameeleza kusikitikishwa na hali hiyo na kuitaka Serikali ya shehiya hiyo kuhakikisha shule hiyo inapata vyoo haraka.

Alieleza kuwa kukosekana kwa vyoo katika shule inapelekea hata maendeleo ya shule kuwa mabovu kwani mara nyingi watoto huwa nje ya eneo la shule.

Alisema huo ni uharibifu wa Mazingira ambao haukubaliki na unatakiwa kuchukuliwa hatua ya haraka ili kuhami Maisha yao.

Aidha Mkuu wa Mkoa ameahidi kuzungumza na wananchi wenye asili ya Mtambwe kuwashawishi kusaidia maendeleo ya shule hiyo .

Shule ya Uwonde imejengwa mwaka 1934 , inakabiliwa na changamoto ya vyoo pamoja na  upungufu wa walimu ambapo kwa sasa inajumla ya walimu 19 na vyumba vya madarasa 22.

No comments:

Post a Comment

Pages