HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

June 26, 2018

VIVUTIO VYA UTALII TANZANIA VYAWAVUTIA WARUSI

BALOZI wa Tanzania nchini Urusi, Meja Jenerali Simon Mumwi, leo ameendesha semina kwa wamiliki wa Kampuni ya Usafirishaji (Tour Guard) mjini Moscow ili kuwapa ufahamu wa vivutio mbalimbali vya utalii vilivyopo nchini Tanzania.

Semina hizo ambazo hufanyikanyika mara moja kila mwezi, zinalenga kuongeza idadi ya watalii kutoka Urusi na nchi za jirani.

Akizungumza katika hafla hiyo, Balozi Mumwi, alisema kuwa semina hizo zimekuwa na manufaa makubwa kwani katika kipindi kifupi zimesaidia sana kuongeza idadi ya watalii wanaotoka Urusi kwenda nchini tanzania, ambapo alisema "katika kipindi cha miaka 10, idadi ya watalii kutoka nchi Urusi imeongezeka kutoka 1500 mpaka 15,000 mwaka huu."
 Balozi wa Tanzania nchini Urusi, Meja Jenerali Simon Mumwi, akinzungumza wakati akifungua semina na siku moja ya kuhamasisha utalii wa Tanzania nchini Urusi, iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Ubalozi, 51 Ulitsa Bolshaya Nikitskaya, Jijini Moscow, nchini Urusi. wanufaika wa semina hiyo walikuwa ni waendeshaji wa huduma za Utalii nchini Urusi. 
Balozi wa Tanzania nchini Urusi, Meja Jenerali Simon Mumwi, akifuatilia mada ya utalii nchini Tanzania, iliyokuwa ikiwasilishwa na Mkurugenzi wa Kampuni ya Safari ambaye ndiye aliyewezesha kuwakutanisha wadau wa masuala ya utalii nchini Urusi, Galina Modestova (kushoto) aliyekuwa akiwasilisha mada hiyo kwa lugha ya kirusi.

No comments:

Post a Comment

Pages