HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

August 10, 2018

NMB YAWANOA AMCOS NANE NANE

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu, Jenesta Mhagama (kulia), akiwakabidhi Meneja Uhusiano Biashara za serikali wa benki ya NMB,Christabel Hiza (kushoto) na Meneja Uhusiano Mwandamizi idara ya Kilimo biashara,Oscar Rwechungura kombe la ushindi wa kwanza taasisi za fedha kwenye kilele cha maonesho ya Kilimo Kanda ya Kaskazini Nanenane Themi mkoa wa Arusha. (Na Mpiga Picha Wetu).

NA MWANDISHI WETU

BENKI ya NMB  imetoa mafunzo kwa zaidi  ya vyama vya msingi 1, 000 vya Ushirika wa Wakulima (AMCOS), yanayohusu kilimo na utunzaji fedha ndani ya mwaka mmoja, yenye lengo la kuboresha sekta ya kilimo nchini.


Akizungumza katika madhimiso  ya kilele cha Sikukuu ya Wakulima ‘Nane Nane’ mkoani Simiyu, Mkurugenzi Mtendaji wa NMB, Ineke Bussemaker, alisema benki yake imemaua kusaidia kuboresha sekta ya kilio kutokana na umuhimu wake katika kuchangia ukuaji wa uchumi wa nchi na pia kuboresha uchumi wa wakulima.


Alisema kuwa, mafunzo hayo ambayo yanaendelea sehemu mbalimbali nchini, yanatarajiwa kuwafikia wakulima wengi zaidi kupitia vyama vya ushirika na hivyo vitawezesha kuboresha kilimo na kuleta mabadiliko ya kiuchumi katika ngazi ya jamii na taifa kwa ujumla.


Bussemaker aliongeza kuwa, sekta ya kilimo ni uti wa mgongo wa uchumi wa nchi na kuajiri Watanzania zaidi ya asilimia 70, hivyo inapaswa kuboreshwa ili kutoa mchango mkubwa katika maendeleo ya kiuchumi.


Alisisitiza kuwa unatakiwa ushirikiano wa wadau mbalimbali wa mendeleo ili kusaidia sekta ya kilimo kukua kwa haraka na kuleta tija kwa wakulima na taifa kwa ujumla na kuwa ikiachiwa serikali peke yake haitaweza kuleta mabadiliko hayo kwa haraka.


Alibainisha ya kwamba benki yake inaamini kuwa sekta ya kilimo ina uwezo mkubwa wa kuleta mapinduzi ya kweli katika uchumi endapo kilimo kitaboreshwa nchini na kwamba itakuwa na mchango mkubwa katika kufikia malengo ya serikali ya uchumi wa viwanda.


Bussemaker alisema kuwa mbali na mafunzo hayo benki yake imekwishatumia zaidi ya Sh. bilioni 100 katika kuboresha sekta ya kilimo nchini kwa kutoa mikopo mbalimbali pamoja na huduma zingine za kifedha kwa wakulima.


“Ndani ya miaka michache ijayo, tunatarajia kutumia kiasi cha Sh. bilioni  500 katika sekta kuwezesha shughuli za kilimo katika mnyororo mzima wa thamani, hivyo nawaomba wakulima kutokata tamaa na kilimo kwani benki  yao ipo pamoja nao katika kuhakikisha inaleta mageuzi ya kilimo kwa manufaa na mendeleo ya wakulima na taifa kwa ujumla” alisema Bussemaker.


Aliwataka wakulima kutumia Benki ya NMB ili kuleta mageuzi chanya katika kilimo na kuinua uchumi wa Tanzania kufikia uchumi wa kati kwa kuzalisha malighafi zaidi ndani ya nchi ambazo zitatumika katika viwanda vilivyopo nchini kwa kuwa mkulima akilima zaidi viwanda vinapata malighafi zaidi.

No comments:

Post a Comment

Pages