HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

August 22, 2018

UN,TEF WATOA MAFUNZO KWA WAANDISHI WA HABARI ZANZIBAR

Na Talib Ussi, Zanzibar
Waandishi wa Habari Visiwani Zanzibar wameshauriwa kuifuatilia na kuiandikia Miradi ya Umoja wa Mataifa (UN) kwa ajili ya kuona faida zake na pia kuibua changamoto zinazojitikeza kwa  maslahi ya Umma.
 Akizungumza katika mafunzo ya siku moja yaliondaliwa kwa pamoja kati ya Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) na Shirika la Umoja wa Mataifa (UN)  na kushirikisha waandishi 20  kutoka Unguja na Pemba kwa niaba ya Ofisi ndogo UN Zanzibar, Mtaalamu wa Uratibu wa Shirika hilo Bi Aine Mushi alieleza kuwa wanahabari ni nguzo muhimu sana katika kufikia malengo ya miradi yao.
Alisema  kuwa UN inadhamira njema kushirikiana na vyombo vya habari ili kuhakikisha vinaelewa na kuandika habari sahihi kuhusiana na miradi ya shirika hilo.
Alieleza kuwa tarehe 28 mwezi huu UN itazindua Pragram maalumu ya pamoja Zanzibar(Zanzibar Joint Proram) ZJP  ambayo itahusisha mashirika 9 ya Umoja huo ambapo Rais wa Zanzibar na Baraza la Mapinduzi atakuwa Mgeni Rasmi.
Alielaza kuwa Program hiyo itajielekeza kwenye maeneo manne ya maendeleo ambayo ni Kupunguza Vifo vya uzazi, Ukatili dhidi ya wanawake na watoto, Uwezeshaji wa Kiuchumi kwa wanawake kupitia zao la Mwani na Uratibu wa Utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo ya Dunia.
“Ili kufanikiwa kwa miradi hii basi ushiriki wa waandishi wa habari ni muhimu sana kwani nyinyi ndio mtakao Ueleza umma nini kimefanyika na nini bado” alieleza Bi Aine.
Mafunzo hayo yalikuwa na lengo ya kujenga Uwezo waandishi wa habari ili waweze kuandika kwa usahihi kazi zinazofanywa na UN na mashirika yake katika eneo la Zanzibar.
Akizungumza kwa niaba ya kikosi kazi cha Mawasiliano cha UN (UNCG), Mchambuzi wa Mawasiliano wa UNFPA, Warren bright alisisitiza umuhimu wa Vyombo vya habari katika miradi ya Umoja huo na kueleza kuwa Vyombo vya habari ni mshirika muhumu katika kazi zao.
“kushirikiana na vyombo vya habari ni suala muhimu kwa UN hapa Zanzibar kwani  wao ndio wanaoweza kupaaza sauti na kuzifikia jamii na kutangaza mafanikio na changamoto za kazi zetu ili na sisi kujiweka sawa” alieleza Bright.

Katibu wa TEF, Neville Meena alisema kuwa Jukwaa hilo limekuwa likifanyakazi na UN kwa miaka mitano sasa na kufahamisha kuwa ushirikiano huo sasa unalenga kuimarisha shughuli zote zinaztekelezwa na pande mbili hizo.
Sambamba na hilo Meena aliwaomba wanahabari hao walioshiriki Mafunzo hayo kuyafanyiakazi kwa vitendo yale yoote waliyoyapata kwa maslahi ya Taifa.
Shirika la Umoja wa Mataifa (UN) kwa upande Zanzibar linatekeleza miradi Zaidi ya 270.

No comments:

Post a Comment

Pages