HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

November 20, 2018

WANAHABARI WALIA NA UCHELEWESHAJI KESI

Dk. Mzuri Issa Ali akizungumza na waandishi wa habari katika kikao maalumu cha kupinga udhalilishaji dhidi ya Wanawake na Watoto Zanzibar.

Na Talib Ussi, Zanzibar

WANAHARAKATI wa kutetea haki za wanawake nchini wametoa wito kwa vyombo vya sheria kuharakisha uchunguzi na kuwaomba pia wananchi kutoa ushirikiano ili kukamilisha kesi za mauwaji ya wanawake na watoto kwa wakati muafaka
Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa Chama cha Waandishi wa habari  wanawake Tanzania (TAMWA) kwa upande wa Zanzibar, Dk  Mzuri Issa Ali katika taarifa yake kwa vyombo vya habari wakati dunia vya ukatili wa kijinsia.inaadhimisha siku 16 za kupinga vitendo

Alieeleza kuwa kama kesi hizo zikishughulikiwa kwa haraka na taarifa zake kusambazwa nchini kote itapunguza tabia ya baadhi ya watu ya kuendelea na tabia hiyo kumaliza maisha ya wanawake na watoto nchi.

Alisema kwa mwaka huu pekee, tayari wanawake watano na watoto wawili wameripotiwa kuuawa katika mkoa wa Kusini Unguja lakini bado kesi hizo hazijapatiwa wowote hadi leo. 

Alieleza kwamba Mei 14, 2018 mtoto Elizabeth Ndaula mwenye umri wa miaka 8 alikutwa amefariki katika kichaka huko Bambi wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja pia Mei 22, 2018 Patima Abdallah Makame (27) na mtoto wake wa miezi mitano Haji Ismail walikutwa wameuawa nyumbani kwao Guruweni Jendele wilaya ya Kati.

Julai 18 na 31, 2018 msichana Wasila Mussa (21) wahuko Tunguu Kichangani Wilaya ya Kati pia mwizi huo huo na Agatha Francis Pius mkaazi wa Kiboje Ndagaa wilayani humo aliuawa kwa kukatwa na kitu chenye makali shingoni kwake wakati akienda shamba saa nne asubuhi.

Novemba 2. 2018 majira ya saa 7:00 usiku Issa Masuli Juma (40) na mkewe Asha Khamis (20) wote wakaazi wa Kibele wilaya ya kati waliuliwa na watu wasiojulikana kwa kupigwa na kitu kigumu sehemu ya kichwani nyumbani kwao.


Dk. Mzuri alieleza kuwa kila wakiwasiliana na jeshi la Polisi wanajibiwa kuwa uchunguzi uendelea na bado haujakamilika na ukamilika watafikishwa mahakamani.

Pia inatoa wito kwa jamii kuacha kabisa vitendo vya kikatili dhidi ya wanawake kwani vinakwenda kinyume na maadili pia na mipango ya nchi ya kimaendeleo.

Hata hivyo kamanda wa Polisi Mkoa wa Kusini Unguja Suleiman Hassan alisema ushahidi unashindwa kupatikana na kutokana na jamii kushindwa kutoa ushirikiano.

“Kwa mfano tukio la mawauji ya Agatha lilitokea mchana kweupe akiwa kondeni, hivi kweli hakuna mtu aliyona mpaka watu kujitokeza kutoa ushahidiii, kwa kweli tunakosa ushirikiano” alieleza Kamanda huyo

Maadhimisho hayo huadhimishwa kila mwaka kuazia  Novemba 25 hadi Desemba 10.

No comments:

Post a Comment

Pages