HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

January 18, 2019

SERIKALI YAGEUKIA UKATILI DHIDI YA WAZEE

Mwakilishi wa Kamishna wa  Ustawi wa Jamii Bw.Ilusubisya Kasebele  akizungumza na wadau wa Ustawi wa Jamii jijini Dodoma wakati akifungua kikao kilicholenga kujadili utekelezaji wa utoaji huduma kwa wahanga wa ukatili katika  Mpango Mkakati wa Kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto.

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imesema mapema mwezi huu itazindua mkakati wa Kitaifa wa kutokomeza mauji dhidi ya wazee ikiwa ni jitihada za  kupambana na ukatili kwa wazee nchini kwani nguvu kubwa imeelekezwa katika ukatili kwa wanawake na watoto.
Hayo yamebainishwa leo jijini Dodoma na Afisa Ustawi wa Jamii Mwandamizi  kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi.Amina Mafita wakati akizungumza katika kikao kilichokutanisha wadau wa ustawi wa Jamii kilichokutana kujadiliana kuhusu utekelezaji wa Mpango Mkakati wa Kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto hasa katika utoaji wa huduma kwa wahanaga wa vitendo hivyo.
Bi. Amina ameeleza kuwa Mpango Mkakati huo wa Kutokomeza Mauaji ya Wazee utasaidia kuinua hari ya wadau katika kuweka nguvu na kutoa elimu kwa jamii kupambana na mauji hayo mabayo mengi yamekuwa yakihusishwa na imani za  kishirikiana katika baadhi ya maeneo  nchini.
Ameongeza kuwa Mkakati huo umeshakamilika na upo tayari na utazinduliwa hivi karibuni ili kuwezesha kutokomeza mauji ya wazee na Mkakati huo ni sehemu yautekelezaji wa Mpango Mkakati wa Kutokomeza Ukatili dhidi ya wanawake na watoto nchini.
“Sasa tumeamua kuangalia na upande wa Wazee kwani nao wanafanyiwa vitendo vya ukatili hasa kuuwawa kikatili  katika maeneo mbalimbali nchini” alisisitiza Bi. Amina.
Kwa upande wake Afisa Ustawi wa Jamii Mwandamizi Bw. Darius Damas  amesema kuwa Serikali inaendelea kushirikiana na wadau katika kuendelea na kupambana na ukatili wa Kijinsia kwani ni watu muhimu katika mapambano hayo.
Amesisitiza  kuwa katika Mpango Mkakati wa Kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake na watoto wadau hao wanakutana kwa lengo maususi la kueleza utekelezaji wa wadau katika utoaji wa huduma kwa wahanga wa vitendo ya ukatili.
Ameongeza kuwa katika kuwezesha utoaji wa huduma kwa wahanga wa vitendo ya ukatili nchini kuna umuhimu wa uwepo wa nyumba salama kwani wengi wanaofanyiwa vitendo vya ukatili ni wanawake na watoto na inasaidia sana kutunza ushaidi wa kesi za ukatili ili kuendelea na  kupambana na Vitendo ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto nchini.
Naye Mwakilishi Shirika la Umoja wa Mtaifa linaloshughulikia Wahamiaji (IMO) Bi. Inna Lutengano  amesema kuwa Shirika lake linashirkiana na Serikali  na Mashirika mengine kutoa elimu kwa jamii kuhusu masuala ya usafrishaji haramu wa binadamu ambapo vitendo hivyo huendana na vitendo vya ukatili na uathiri sana wanawake na watoto.
Kwa upande wake Mwakilishi wa Shirika la Railway Children Africa Bi. Mary Katama amesema kuwa Shirika lao limejikita katika kuwasaidia watoto wa mitaani na wengi wao wakiwa wamekimbia sehemu wanazoishi kutokana na vitendo vya ukatili dhidi yao.
Ameeleza  kuwa wamekuwa wakitoa nafunzo kwa watoto na wazazi kuhusu malezi bora na kuhakikisha kuna usalama katika familia ndipo huwarudisha watoto hao katika familia zao na kwa wale walio na umri kuanzia miaka 15 wanawapatiwa stadi za kazi ili kujiendeleza na kujitegemea.
Kikosi kazi cha utekelezaji wa Mpango Mkakati wa Kutokomeza Ukatili dhidi ya wanawake na Watoto (MTAKUWA) kwa upande wa utoaji wa huduma kwa wahanga wa vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto kiekutana jiji ni Dodoma ikiwa ni miongoni mwa vikao vya kila mara wanavyokutana kupeana mrejesho wa utekelzaji wa majukumu yake.

No comments:

Post a Comment

Pages