HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

February 12, 2019

VIFO VYA AKINA MAMA NA WATOTO WACHANGA VYAPUNGUA ZNZ

Na Talib Ussi

Wizara ya Afya Zanzibar imesema Vifo vya akina mama na watoto wachanga katika Visiwa vya Zanzibar vimepungua kutoka vifo 237 hadi kufikia 219 kwa mwaka 2015-17.

Hayo yamebainika leo  katika kikao cha Baraza la wawakilishi Chukwani nje kidogo ya Mji wa Zanzibar, Naibu Waziri wa afya Zanzibar Harusi Saidi Suleiman wakati ajibu swalila mwakilishi wa Chake Chake Suleiman Sarahan Said.

Mwakilishi huyo aliuliza swali Je, suala la uzazi  salama kwa akinamama na mtoto ni tatizo kubwa au kama limepungua kwa asilimia ngapi.

Naibu huyo  alilieleza bara kuwa   kwa sasa hali ya Vifo kwa kina mama imepungua ambapo kwa upande wa watoto wachanga pia vimepungua kutoka vifo 79 hadi kufikia vifo 56 kati ya vizazi hai laki moja kwa mwaka 2015-17.


Alifahamisha kuwa kwa sasa Wizara yake imeamua kuimarisha upatikanaji wa huduma muhimu kwa wazazi  ili kujinga na tatizo la vifo vya kina mama na watoto wachanga.

“Serikali inaendelea na azma yake ya kuimarisha miundombinu ya huduma za afya kwa wananchi  pamoja na kuendelea kutoa elimu ya afya ili wananchi hususan kina mama wajawazito waweze kujifungua salama” alieleza Naibu Harusi.


Sambamba na hilo alieleza kuwa  Wizara inaendelea kufanya tafiti mbalimbali za kiafya ikiwemo kufanya utafi na kutathmini huduma za dharura wakati wa ujauzito,Wakati wa kujifungua na watoto wachanga ili kumuandalia mama mjamzito mazingira bora ya kujifungua salama.


Akizungumzia sababu zinazochangia vifo vya kina mama na Watoto wachanga alisema  ni pamoja na  uhaba wa elimu ya Afya hususan Maskulini ,imani potofu katika jamii  pamoja na lishe duni kwa mama na mtoto.


“Miundombinu mibovu wa Barabara jambo ni sababu nyengine kubwa jambo ambalo linawapa wakati mgumu wazazi wakati  wakitaka kuvifikia vituo vya Afya na kushindwa kupata huduma kwa haraka” alieleza Bi Harusi.


No comments:

Post a Comment

Pages