HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

February 19, 2019

WATEJA WA HALOTEL KUPIGA SIMU, KUTUMIA INTANETI BILA KIKOMO

 Mkurugenzi Mkuu wa Halotel Tanzania, Nguyen Van Trung, akizunguka wakati wa uzinduzi wa huduma mpya za Royal Bundle na Tomato Bundle uliofanyika jijini Dar es Salaam leo Feb, 19, 2019.
Mkurugenzi Mkuu wa Halotel Tanzania, Nguyen Van Trung, akizungumza katika hafla hiyo.
 Wageni waalikwa, wasanii mbalimbali pamoja na wafanyakazi wa Halotel wakiwa katika hafla hiyo.

Mkuu wa Mawasiliano wa Halotel, Mhina Semwenda, akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa huduma mpya za Royal Bundle na Tomato Bundle uliofanyika jijini Dar es Salaam leo Feb, 19, 2019. Kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Masoko wa Halotel, Do Le Hoan na katikati ni Mkurugenzi Mkuu wa Halotel Tanzania, Nguyen Van Trung.

Mkuu wa Mawasiliano wa Halotel, Mhina Semwenda, akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa huduma mpya za Royal Bundle na Tomato Bundle uliofanyika jijini Dar es Salaam leo Feb, 19, 2019. Kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Masoko wa Halotel, Do Le Hoan na katikati ni Mkurugenzi Mkuu wa Halotel Tanzania, Nguyen Van Trung.

Wafanyakzi wa Halotel pamoja na wadau mbalimbali wakiwa katika hafla hiyo.

Baadhi ya wasanii na watangazaji waliohudhuria hafla hiyo.

Baadhi ya maofisa wa Halotel wakiwa katika uzinduzi huo.

Kabla ya uzinduzi.

Mkurugenzi Mkuu wa Halotel Tanzania, Nguyen Van Trung, akiteta jambo na Ofisa Uhusiano wa Halotel, Stellah Pius.

Mkurugenzi Mkuu wa Halotel Tanzania, Nguyen Van Trung akijadiliana jambo na Mkuu wa Mawasiliano Halotel, Mhina Semwenda.

Mkuu wa Mawasiliano wa Halotel, Mhina Semwenda (kushoto) na Ofisa Uhusiano wa Halotel, Stellah Pius.
 Mkurugenzi Mkuu wa Halotel Tanzania, Nguyen Van Trung,akisalimiana na msanii wa Bongo Fleva, Mr. Blue.
 Mkurugenzi Mkuu wa Halotel Tanzania, Nguyen Van Trung,akijaribu kufungua Champagne.
Mhina Semwenda akifungua Champagne.
Mkurugenzi Mkuu wa Halotel Tanzania, Nguyen Van Trung (wa pili kushoto). akigonga tano na Mkuu wa Mawasiliano wa Halotel, Mhina Semwenda pamja na wasanii waliohudhuria hafla ya uzinduzi wa huduma mpya za Royal Bundle na Tomato Bundle.

Na Mwandishi Wetu

KAMPUNI ya Mawasiliano ya Simu za Mkononi ya Halotel imeanzisha huduma mbili mpya zijulikanazo kama Royal Bundle na Tomato Bundle, zote zikilenga kumrahihishia mteja katika huduma za kupiga simu pamoja na intaneti kwa gharama nafuu.

Akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa huduma hiyo Jijini Dar es Salaam jana, Naibu Mkurugenzi wa Halotel, Nguyen Van Truang alisema huduma hizo pia zimelenga kuongeza ubora katika utoaji wa huduma za simu kupitia mtandao huo hapa nchini.

Alisema huduma ya Royal Bundle, imeanzishwa kama moja ya ubunifu wa kukata kiu ya wateja ambao walikuwa wanatamani kutumia huduma bila kupata shida ya aina yoyote ikiwemo ya kuisha muda wa maongezi au intenet kukata wakati wakiendelea kuongea au kuperuzi.

“Tunatambau umuhimu wa sekta ya mawasiliano katika shuhuli za kiuchumi hivyo tusingependa kampuni yetu kikwazo katika kulifanikisha hilo na ndiyo maana leo tunawatangazia huduma wa huduma hizo nchini” alisemaTruang.

Aliongeza kuwa kupitia huduma hiyo kwa sasa watumiaji wa mtandao wa Halotel kwa kiasi cha Sh 10,000 wanaweza kupiga simu za ndani na za kimataifa kwa nchi za Marekani, China,Canada,India na zinginezo sambamba na kutuma sms bila kikomo .

Alisema faida zingine kwa mtumiaji wa mtandao huo ni pamoja na kujipatia muda wa maongezi wa dakika 520 kwa Sh 10,000 atakayokuwa ameiongeza katika simu yake ambazo zitamuwezesha kupiga simu kwenda mitandao yote pamoja na kuwezeshwa kifurushi cha inteneti cha GB 2.

Aidha kuhusu kifurushi cha Tomato Bundle, Naibu Mkurugenzi huo alisema kupitia huduma hiyo, mteja na watumiaji wa Halotel nchi nzima wataweza kupiga simu halotel kwenda halotel kwa dakika tano bure za mwanzo katika kila simu atakayopiga pamoja na kupata salio la Sh 4000 ambalo atalitumia kwenye huduma nyingine za Halotel kwa kipindi cha mwezi mzima.

No comments:

Post a Comment

Pages