HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

March 31, 2019

Timu ya Vijana ANOCA yaenda Rwanda na matumaini kibao

NA MWANDISHI WETU


KIKOSI cha Timu ya Tanzania inayotarajiwa kushiriki michezo ya Vijana ya Kamati za Olimpiki Afrika (ANOCA), Zone 5 jijini Kigali Rwanda, imeondoka jijini Dar es Salaam jana ikiwa na matumaini kibao.

Timu hiyo inayoundwa na michezo ya Kikapu na Riadha, iliondoka jana amjira ya saa 11:30 jioni na ndege ya Shirika la Rwanda, ikiwa chini ya Mkuu wa msafara, Shehe Mohamed Ali kutoka KMKM Zanzibar.

Akizungumza muda mfupi kabla ya kukwea pipa, Kocha wa Riadha, Mwinga Mwanjala, alisema vijana wake wanakwenda kupambana kadiri ya walivyojiandaa.

“Tunakwenda kupambana kulingana na jinsi tulivyojiandaa, tusubiri siku ya tukio tuone vijana wanaamkaje, tuombe vijana wawe na afya njema wapambana kadiri ya uwezo wao ili kufanya vizuri,” alisema Mwinga.

Naye Kocha msimamizi wa timu ya Kikapu, Phineas Kahabi, alisema walikuwa kambini kituo cha michezo cha Filbert Bayi, Mkuza Kibaha hadi jana na wamejiandaa vema.

“Tulikuwa na muda mwingi wa kujiandaa, vifaa na huduma ikiwamo malazi ilikuwa nzuri…Shukrani kituo cha Filbert Bayi na Kamati ya Olimpiki kwa ujumla, vijana wako vizuri mentally na physically, hivyo hatuna visingizio,” alisema Kahabi.

Kocha huyo, alifafanua kuwa kikosi chake kinaundwa na wachezaji wanne na wanakwenda kucheza mchezo wa wachezaji watatu  watatu ‘3x3’ huku wakitumia nusu kiwanja.

Kahabi, alitoa hofu Watanzania kuhusiana na mchezo huo ambao bado haujaenea sana hapa nchini, kwamba vijana wake walishaanza kuucheza toka mwaka jana, hivyo wamejiandaa kimwili na kiakili na kwamba amekuwa akiwakumbusha mara kwa mara sheria za mchezo huo, kwani ni tofauti na zile za Kikapu za kawaida.

Timu hiyo inaundwa na Wanariadha Regina Mpigachai (Mita 800), Amos Matondo (Mita 400), Esther Martin (Mita 1,500), na Gaudensia Maneno (Mita 800).
Kwa upande wa Kikapu ni Daud Maiga (Nahodha), Josephat Sanka, Ally Abdallah na Charles Mayombo.

No comments:

Post a Comment

Pages