HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

March 31, 2019

WASANII BARNABA, TABU KUONGOZA MBIO ZA SELOUS

Angela Karashana, ambaye alimwakilisha Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe, akizungumza kuhusu  mbio za Selous 2019, zitakazofanyika mkoa wa Morogoro.


NA MWANDISHI WETU

Msanii wa Bongo Fleva nchini, Barnaba Eliasa 'Barnaba Boy', pamoja na Msanii wa vichekesho Tabu Mtingita, kuongoza mbio za Selous Marathon zitakazo fanyika  Agosti 24 mkoani Morogoro.

Akizungumza kwa niaba ya waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe, Angela Karashana alisema kuwa mchezo wa riadha unamahusiano makubwa na burudani uwezi kucheza au kukimbia bila kuburudika ndio sababu tunawaona wasanii wako kwa kuweza kutuburudisha tunapomaliza kukimbia. 

"Mtoto anapokuwa tumboni mama lazima uulizwe mwanao anacheza tumboni, kwa kuwa kucheza kuna hashiria uhai, Wapo watu wanatamani wapate nafasi ya kutembea tu na hawapati wewe mwenye nafasi hii unaitajika kushiriki mbio za Selous 2019 kuna Wat u watashangaa kwa nini Barnaba na Tabu wanashiriki ni kutokana na kuwa watu wanakimbia umbali mrefu watu wa rika tofauti na wakimaliza kukimbia wanaitaji kutuburudisha na kufurahia walichokifanya mbio zitafanyika Morogoro Watu wajitokeze tukimbie kwa pamoja na michezo mbalimbali itakuwepo"anasema Karashana.  

Kwa upande wake mkali huyo wa Bongo Fleva anasema yupo tayari kukimbia na watu wa Morogoro leo tumezindua rasmi kadri tunavyoendelea watu wafate taratibu na kujiandikisha kushiriki mbio hizi ili tuweze kukimbia na kuburudika kwa pamoja.

No comments:

Post a Comment

Pages