HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

April 08, 2019

Dimpoz awafanyia kufuru mashabiki zake

Nyota wa muziki wa kizazi kipya, Ommy Dimpoz, akichagua viatu katika duka la GSM Mall lililopo Barabara ya Pugu jijini Dar es Salaam, mwishoni mwa wiki. (Picha na Francis Dande).  




Baadhi ya vitu vinavyopatikana katika duka la GSM Mall Pugu Road.

NA JOHN MARWA
NYOTA wa muziki wa Bongo Fleva Ommy Dimpoz anayetamba na kibao chake cha ‘You Are The Best’ amewapigisha pamba mashabiki zake katika duka la GSM Mall Pugu ukiwa ni muendelezo wa kutoa zawadi kwa mashabiki zake.
Washindi wawili mmoja wa kiume Charles Allen na wakike Sarahati Rashid wameibuka washindi kwa mujibu wa Dimpoz baada ya kupitia posti za mashabiki zake wanatumia muda wao mwingi kuposti kazi zake.
Akizungumza na waandishi wa habari katika duka la GSM Mall ambalo aliwafanyia shoping, Nyota huyo kutoka Rock Star alisema alifurahishwa na jinsi Charles na Sarhati walivyotoa mchango mkubwa kusapoti kazi zake.
“Nimeangalia ni shabiki yupi anamchango mkubwa wa kusapoti kazi zangu nikagundua kuwa Charles na Sarhati wamekuwa wanajitoa sana kusapoti kazi zangu, japo wapo wengi wanaofanya kama wao.
“Nimewachagua mwenyewe kuwawakilisha mashabiki zangu wengine kwa hiki kidogo lakini chenye hadhi, kwa kushirikiana na GSM Mall nimeamua kuwafanyia shoping kwa kuzingatia jenda japo sio mara ya kwanza na ya mwisho nadhani nimeanza na hawa kama nyimbo yangu inavyosema you are my best.
“Ni kweli sijawahi kufanya kitu kama hiki lakini ni vizuri vile tunavyovipata tugawane na marafiki na mashabiki si kitu kibaya wanapenda, yawezekana siku Mungu akijalia tukipata kikubwa zaidi kuna siku labda ntatoa gari yote kheri,”alisema

No comments:

Post a Comment

Pages