HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

April 10, 2019

Karia aomba amshaamsha kuwachakaza wapinzani Afcon U17

NA JOHN MARWA
 
RAIS wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Wallace Karia ameiomba kamati ya hamasa kwa timu ya taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' kugeukia upande wa timu ya taifa chini ya miaka 17 (Serengeti Boys).
Serengeti Boys ambao ni wenyeji wa fainali za mataifa ya Afrika kwa vijana wenye umri huo ambazo zitafanyika kwa mara ya kwanza hapa nchini kuanzia Aprili 14 hadi 28 mwaka huu.
Karia ameiomba kamati hiyo iliyoko chini ya mwenyekiti wake Paul Makonda, kuhamishia hamasa kwa Serengeti Boys ili waweze kuweka historia nyingine kwenye soka la Tanzania kwa kubakiza taji hilo ama kupata naafasi ya kufuzu fainali za Dunia nchini Brazili.
"Namuomba mheshimiwa Makonda alibebe hili nalo ili kama nchi tuweze kuipeperusha vema bendera ya Tanzania, naamini inawezekana kwa maslahi mapana ya taifa.
"Lengo letu ni kutwaa uchampion kwa faida ya kuwa wenyeji lakini kama itashindikana japo hilo la kushindwa halipo kichwani mwetu basi tupate nafasi ya kwenda kombe la dunia," alisema Karia na kuongeza kuwa.
"Ni wazi  muda ni mchache uliosalia  lakini hakuna budi kushikana mikono na kulibeba tukio zito lililopo mbele yetu."

No comments:

Post a Comment

Pages