HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

April 10, 2019

TFF, AZAM TV NA SERIKALI KULA SAHANI MOJA NA VISHOKA WEZI WA MATANGAZO

                                    NA JOHN MARWA

SHIRIKISHO la Soka Tanzania TFF kupitia Rais wake Wallece Karia, amesema ukiukwaji wa haki za kurusha matangazo kwa michezo ya Ligi Kuu na Kombe la Azam FA, linachangia kuikosesha Serikali mapato.
Hatua hiyo imekuja mara baada ya hivi karibuni kuibuka Luninga zenye Cable ambazo zinakiuka utaratibu huo  jambo ambalo linaingilia haki za mwenye mkataba wa kisheria kutoa huduma hiyo.
Karia amewataka wanaohusika na michezo hiyo kuacha mara moja kwani aliyepewa haki  ya kurusha matangazo hayo ni Azam Tv na amekuwa akilipa kodi kwa wakati kama ambavyo walivyokubaliana kwenye mkataba wao.
Amesema hali hiyo inasababisha ligi hiyo kukusa udhamini Mkuu  hivyo wameona watoe onyo hilo kwa wote wanaofanya vitendo hivyo kuacha mara moja kuepuka kuchukuliwa hatua za kisheria kumlinda mdhamini mzawa aliyejitokeza kudhamini ligi hiyo.
“Siku za hivi karibuni kumejitokeza wimbi kubwa la Luninga za Cable ambazo zinaiba matangazo kutoka Azam na wanaonesha bila kufanya makubaliano na aliyepewa haki au TFF jambo ambalo linaweza kusababisha Azam ambao ni wadhamini kujitoa kwa kukosa mvuto.
TFF hatuna mkataba wowote na Luninga za Cable kuendelea kufanya hivyo wanakiuka kanunini na sheria zilizowekwa  hivyo tunatarajia kwenda Mahakamani kufungua kesi wanaohusika kufanya jambo hili wakamatwe wafikishwe kwenye vyombo vya dola,  amesema Karia na kuongeza kuwa.
“Ukiukwaji huo hadi sasa umesababisha  athari kubwa ikiwemo serikali kupoteza mapato na Azam kama mdhamini aliyeuziwa haki ya matangazo hayo kudhoofisha uchumi wake,”.
Alisema ili kuhakikisha wanadhibiti jambo hili ambalo linachangia kurudisha nyuma watu wenye uwezo kuwekeza kwenye mchezo wa soka, wameunda kamati kutoka TFF, Azam Media na Jeshi la Polisi kwa ajili ya kuwakamata wote ambao wanafanya hivyo kuwapeleka kwenye vyombo vya dola.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Azam Tv Tido Muhando alisema hata kwa watu wanaorusha matangazo hayo kwa njia ya You tube  ni kinyume na makubaliano na kwamba hiyo ni biashara kama biashara zingine hivyo lazima utaratibu uheshimiwe kwa maslahi mapana ya maendeleo ya soka nchini.
“Nawapongeza TFF,kwa kuliona hilo jambo ambalo limekuwa likituumiza kichwa kwa kiasi kikubwa na kuwaomba wanaofanya hivyo waache mara moja na kuheshimu taratibu na kanuni zilizowekwa” amesema Tido.

No comments:

Post a Comment

Pages