HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

April 12, 2019

MOI YAENDESHA KAMBI KUBWA YA UPASUAJI BUGANDO

Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Dk. Philis Nyimbi, akizungumza na waandishi wa Habari (hawapo pichani) katika hafla ya kufunga kambi ya upasuaji wa Ubongo, Mgongo na Mishipa ya Fahamu iliyofanyika Bugando.
Mkurugenzi Mtendaji wa MOI Dkt Respicious Boniface akieleza namna MOI ilivyojipanga kusogeza huduma kwa wananchi kwa kufanya kambi za uapasuaji, katika hafla ya kufunga kambi ya Upasuaji wa Ubongo, Mgongo na Mishipa ya Fahamu iliyofanyika Bugando
  Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya rufaa ya Bugando Profesa Makubi akitoa taarifa ya namna kambi ya upasuaji iliyoendeshwa kwa ushirikiano kati ya MOI, Bugando na Cuba ilivyofanikiwa.
Madaktari Bingwa wa MOI, Cuba na Bugando wakifanya upasuaji mkubwa wa mgongo katika hospitali ya Bugando jijini Mwanza. (Na Mpiga Picha Wetu).

 Mwanza, Tanzania
Zaidi ya wagonjwa 400 wamehudumiwa kati yao 17 wakifanyiwa upasuaji mkubwa na jopo la madaktari bingwa wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa MOI, Cuba na Bugando katika  kambi ya upasuaji wa Ubongo, Mgongo na Mishipa ya fahamu katika Hospitali ya rufaa ya Bugando Mwanza toka tarehe 8/04/2019 hadi 12/04/2019.

Akihitimisha kambi hiyo Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Dkt Philis Nyimbi amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kwa kufanya maboresho makubwa hapa nchini hususani kwenye huduma za Afya. 

"Kambi hii ya upasuaji wa Ubongo, Mgongo na mishipa ya fahamu imewezakana kutokana na Maboresho yaliyofanywa na Serikali ya awamu ya Tano, kwa niaba ya mkuu wa Mkoa wa Mwanza Ndugu John Mongela tunawashukuru wakurugenzi wakuu wa MOI na Bugando pamoja na madaktari Bingwa wote, kwa hili wananchi wa kanda ya ziwa wamenufaika sana" Alisema Dkt Nyimbi.

Mkurugenzi Mtendaji wa MOI Dkt Respicious Boniface amesema hii ni sehemu ya mkakati wa MOI na Serikali wa kuhakikisha huduma za kibingwa zinawafikia wananchi wote hususani wa mikoa ya pembezoni.

“Baada ya Serikali kufanya uwekezaji mkubwa MOI ,rufaa za nje ya nchi zimepungua sana ,hivi sasa mpango wa MOI na Serikali ni kuhakikisha huduma za kibingwa zinawafikia wananchi wote.” Alisema Dkt. Boniface.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Bugando  Profesa Abel Makubi ameushukuru Uongozi wa MOI kwa kukubali kuleta madaktari Bingwa Mwanza ambao wamewahudumia wakazi wa kanda ya ziwa na kuwapunguzia adha ya kusafiri kwenda Dar es Salaam au nje ya nchi.

“kwa niaba ya bodi  pamoja na menejimenti ya Hospitali ya Bugando tunawashukuru wenzetu wa MOI,Cuba kwa kuja kushirikiana nasi hapa kwenye kambi hii, tunaamini huu ni mwanzo wa ushirikiano baina ya taasisi zetu wakazi wa kanda ya ziwa wataendelea kunufaika" Alisema Profesa Makubi.

Taasisi ya MOI imekuwa ikitekeleza kwa vitendo maagizo ya Serikali ya kuhakikisha inawaogezea wananchi wa mikoa ya pembezoni huduma za kibingwa ili kuwapunguzia adha kusafiri kuzifuata huduma hizo MOI. 

No comments:

Post a Comment

Pages