HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

April 08, 2019

OMMY DIMPOZ: SIMBA BADO WANANAFASI YA KUFANYA VIZURI, WATANZANIA WAJITOKEZE KUWAPA SAPOTI SERENGETI BOYS AFCON U 17


NA JOHN MARWA

LICHA ya suluhu waliyoipata Simba SC katika mchezo wao wa kwanza wa robo fainali Ligi ya Mabingwa Afrika CAF CL jumamosi iliyopita dhidi ya TP Mazembe Nyota wa Bongo Fleva ambaye ni shabiki mkubwa wa klabu hiyo Ommy Dimpoz bado anaamini watapenya nusu fainali.

Dimpozi amesema watu wasiichukulie poa Simba kwani mpira una maajabu yake hivyo wanapaswa kutunza maneno yao na kusubiri dakika 90 za Lubumbashi.

Simba walitoka sare ya kwanza msimu huu katika Uwanja wa Taifa wakitoka kushinda mechi tano mtawalia kabla ya kuzuiwa na Mazembe kwa kushindwa kupachika bao mbele ya miamba hiyo ya Afrika.

Lilikuwa ni pambano la kwanza na mtanange wa pili utapigwa siku ya jumamosi mjini Lubumbashi nchini Congo DR nyumbani kwa TP Mazembe ambao watahitaji ushindi ili kusonga mbele.

Simba licha ya kuhitaji ushindi katika kabumbu hilo la marejeano kama watapata sare ya mabao kwao utakuwa ni ushindi utakao wapeleka nusu fainali japo sio kazi nyepesi dhidi ya mabingwa hao mara tano wa michuano hiyo.

Akizungumza jijini Dar es Salaam Omary Nyemo Ommy Dimpoz alisema lolote linawezekana katika mchezo wa soka hivyo anaamini Simba inaweza kupata matokeo na kusonga mbele kama watatimiza majukumu yao kikamilifu.

“Kama wao walijipanga na kuweza kupata sare na sisi tunaweza kujipanga na kupata ushindin Lubumbashi, tunaamini tunacheza na klabu kubwa katika haya mashindano pia wao ni mabingwa mara tano hivyo wanauzoefu na hii michuano.

“Mwanzo lengo la Klabu lilikuwa kufika hatua ya makundi lakini tumevuka lengo tumefika hataua ya robo fainali bado tunaamini tutajipanga mpira ni dakika 90 kuna watu hawakutegemea Simba kufika hapa lakini wako wapi, Alhy kapigwa tano huko sio kwamba hajui ndo mpira. Alisema na kuongeza kuwa,”alisema na kuongeza kuwa.

“Penati anakosa mtu yeyote wanakosa akina Messi na Ronaldo kwanini watu wamlaumu Bocco inawezekana ikatugahrimu lakini ndio mpira.

“Yawezekana tungeshinda 4-0 hapa na kule tukapigwa 5-0 tusingeweza kusonga mbele lakini yawezekana tukawafunga bao moja kwao na wakashindwa kuchomoa na Simba kusonga mbele.

“Katika hatua hii lazima mmoja atoke hivyo hata kama tutatoka ndio mpira ila Imani yangu ni kubwa sana Simba tunaweza kusonga mbele.

Aliongeza kuwa mafanikio ya Simba yameweza kuliinua soka la Tanzania yamerejesha hamasa kwa watanzania, na wameanza kujiamini kuwa timu zao zinaweza kupata matokeo mazuri kama ambavyo imekuwa kwa  Taifa Stars kufuzu AFCON.

Pia alitoa rai yake kwa watanzania kuelekea mashindano ya vijana ya afrika ambayo Tanzania ni wenyeji kupitia Serengeti Boys 

“Kuna umuhimu wa kujitokeza kwa wingi kutoa hamasa kwa vijana wetu lakini pia kama nchi tukijitokeza kwa wingi inaweza kutujengwea Imani na kupewa nafasi nyingine kwa michuano mikubwa zaidi hivyo hii ni fursa itumike vema  vema.

“Michuano hii itatufanya tutembee vifua mbele kwenye mataifa ya watu tukijivunia kuandaa michuano mikubwa ya AFCON kwa vijana Afrika,”alisema.

No comments:

Post a Comment

Pages