HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

April 04, 2019

WIKI YA TANO YA TAFITI YA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM NGAZI YA NDAKI, SHULE KUU NA TAASISI

Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kupitia Ndaki, Shule Kuu na Tasisi zake imeonesha tafiti zilizofanywa na wanataaluma, pamoja na wanafunzi wake ili tafiti hizo zitumike kutatua changamoto zilizopo nchini hususani katika suala zima la maendeleo. 

Tafiti hizo ambazo zimeoneshwa katika Kampasi ya Mwalimu Nyerere, Chuo kishiriki cha Elimu cha Dar es Salaam (DUCE), Shule Kuu ya Uandishi wa Habari na Mawasiliano ya Umma (SJMC) pamoja na Ndaki ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (CoICT) zimefanyika kwa siku mbili kuanzia tarehe 3 na 4 Aprili 2019.

Katika maonesho hayo, wadau na wanafunzi kwa ujumla wametembelea mabanda na kujifunza masuala mbalimbali kutoka kwa wahadhiri na wanafunzi wa shahada za awali na zile za juu.  

Kauli mbiu ya wiki ya Tano ya Tafiti hizo Ni “Utafiti kwa Maendeleo Jumuishi na Endelevu” inatarajia kukamilika Tarehe 6 hadi 8 Mei, 2019 kwa maonesho ya jumla ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Naibu Makamu Mkuu Tafiti na Maarifa wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Prof. Cuthbert Kimambo (mwenye Tai) akiwa na Mkurugenzi wa Tafiti na Uchapishaji Dkt. Pendo Balangwa wakipokea maaelezo kutoka kwa wataalamu wa Ndaki ya Uhandisi na Teknolojia (COET) walipotembelea banda lao Katika Kampasi ya Mwalimu Nyerere Jijini Dar es Salaam.
 Naibu Makamu Mkuu Tafiti na Maarifa wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Prof. Cuthbert Kimambo (mwenye Tai) akiwa na Mkurugenzi wa Tafiti na Uchapishaji Dkt. Pendo Balangwa wakiangalia na kupokea maelezo ya mtambo wa kupoza hewa kutokwa kwa mmoja wa wanafunzi wa shahada ya juu katika Ndaki ya Uhandisi na Teknolojia (COET) katika wiki ya Tafiti ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Pages