HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

June 06, 2019

ONYESHO LA EID AL FARIS KUUNGURUMA IJUMAA JUNI 7 DAR ES SALAAM

Mratibu wa Onyesho la muziki lijulikanalo kama ‘The Eid Al Faris 2019", Antonio Nugaz, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo Juni 6, 2019, wakati wa kutambulisha onyesho hilo. 
 Mkurugenzi wa Van Mo Company Ltd, Abdul Mohamed, akifafanua jambo wakati wa kutambulisha kwa waandishi wa habari onyesho la "Eid Al Faris 2019" litakalofanyika Juni 7, 2019 kwenye hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi wa Van Mo Company Ltd, Abdul Mohamed, akifafanua jambo.
 Sheikh Masoud Feruzi kutoka Nasaha Crew akizungumza na waandishi wa habari kuhusu ushiriki wa kundi lao katika onyesho hilo.
 Msanii wa Komedi kutoka nchini Kenya, Sammy Kioko, ambaye naye atakuwepo katika onyesho hilo.
 Msanii wa Komedi kutoka Kenya, Nasra Yusuph, akizungumzia onyesho hilo.
 Picha ya pamoja.


Na Mwandishi Wetu

KAMPUNI ya Kitanzania ya Van Mo Company Ltd ya jijini Dar es Salaam, imetambulisha Onyesho kubwa na la aina yake la muziki lijulikanalo kama ‘The Eid Al Faris 2019, linalofanyika Ijumaa hii Juni 7, kwenye Hoteli ya Serena, jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa Mratibu wa onyesho, Antonio Nugaz, Eid Al Faris ni jukwaa la aina yake kuwahi kufanyika nchini Tanzania, litakalojumuisha burudani mbalimbali, ikiwemo vichekesho, nyimbo za dini (Qaswida), sambamba na chakula cha usiku.

Nugaz alibainisha ya kwamba, matamasha kama hayo ni utamaduni uliozoeleka sana miongoni mwa Waislamu na jamii za watu wa Mwambao, hususani katika kipindi cha Sikukuu ya Eid el Fitr, huku akiwataka Watanzani kujitokeza kushuhudia burudani hizo ndani ya Eid Al Faris.

Alifafanua ya kuwa, Eid Al Faris litapambwa na burudani kutoka kwa Wakali wa Qaswida wa Kundi la Nasaha, huku Sitti and The Band, ikialikwa kutumbuiza katika mahadhi, mirindimo na maudhuhi ya Qaswida. 

“Pia kutakuwa na vichekesho kutoka kwa mastaa wa Komedi kama vile Nasra na Sammy Kioko kutoka Nairobi, Kenya, ambako viingilio vitakuwa ni Sh. 50,000 (bila chakula), Sh. 100,000 (pamoja na chakula) na Sh. 130,00 (sambamba na huduma za ziada za ki-VIP).

Naye Mkurugenzi wa Van Mo Company Ltd, Abdul Mohamed, alisema Eid Al Faris 2019 limeratibiwa na kampuni yake hiyo, huku likiwezeshwa na Kampuni za GSM Africa, Superdoll, VIMTO na ASAS Group, huku Clouds Fm (wakiwa ndio Official Radio partner) na Azam TV (official broadcaster and TV patners). 

No comments:

Post a Comment

Pages