HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

August 20, 2019

Marufuku uuzaji Vipepeo yaleta umaskini Amani


NA SULEIMAN MSUYA
UAMUZI wa Serikali kuzuia uvunaji viumbe hai wakiwemo Wadudu aina ya Vipepeo katika Kijiji cha Shebomeza, Kata ya Amani Wilayani Muheza mkoani Tanga umetajwa kusababisha umaskini kijijini hapo.
Hayo yamesemwa na viongozi wa kijiji cha Shebomeza na Kata ya Amani wakati wakizungumza na Blog hii hivi karibuni.
Mwenyekiti wa Kijiji cha Shebomeza, HamisI Barua alisema mradi wa Vipepeo ulianza kuleta mabadiliko ya maisha ya wananchi wake kwa kupata kipato kinachokidhi mahitaji yao.
Barua alisema Kipepeo alikuwa anaingiza kipato kuliko hata mfugaji ambapo kiwango kidogo mfugaji alikuwa anaingiza zaidi ya shilingi 500,000.
“Mimi kama Mwenyekiti wa kijiji nadiriki kusema kuwa uamuzi wa Serikali hauna tija kwa wananchi kwani ufugaji wa Vipepeo hauna athari kwa mazingira na viumbe hao kwa kuwa utaratibu unafuatwa,” alisema.
Alisema kutokana na uamuzi huo wananchi wengi wameshindwa kushiriki kuchangia huduma za kijamii kwa kukosa kipato.
Mwenyekiti huyo alisema Vipepeo wana soko kubwa nje ya nchi hivyo ni lazima Serikali kutafakari upya ili wananchi waweze kuendelea na uzalishaji wa viumbe hao.
Mtendaji wa Kijiji cha Shebomeza, Michael Siafu, alisema Serikali inapaswa kuja na majibu ya kitafiti ni hasara gani wamepata kutokana na ufugaji huo wa Vipepeo ndi watoe maamuzi.
Ofisa Mtendaji wa Kata Amani, Hadija Nassoro (pichani), alisema uamuzi wa Serikali kuzuia ufugaji na uuzaji wa Vipepeo ulikuwa wa haraka hali ambayo inachangia jamii kurejea katika maisha ya kusubiri misaada wakati walianza kujikomboa kiuchumi.
“Mimi na ugeni wangu lakini naona ni vizuri Serikali ikajitafakari umpya kwani Vipepeo huwa vinazalishwa ndani ya uzio maalumu na ni lazima mazingira yawe mazuri ndio wanazaliana,” alisema.
Meneja Mradi wa Vipepeo, kutoka Shirika la Kuhifadhi Misitu ya Asili Tanzania (TFCG), Amir Said alisema kimsingi uamuzi wa Serikali kuzuia biashara hiyo hauna faida kwa nchi wala wananchi na kusisitiza kuwa miradi inayoibuliwa vijijini haina dhamira ya kuharibu mazingira.
“Tumewafundisha wananchi namna ya kuzalisha vipepeo kwa kutumia eneo dogo ambapo wanawrka nyavu na uchumi wa wananchi ulianza kuimarika,” alisema.
Jana akijibu maswali ya viongozi na wananchi wa vijiji vinazalisha Vipepeo Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Martin Shegela aliwataka wananchi hao kuwa na subira wakati Serikali inaendelea na mchakato utakaotoa majibu sahihi ya nini kifanyike.

No comments:

Post a Comment

Pages