HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

August 20, 2019

MSHIRIKI SADC AIFAGILIA MOI

NA ASHA MWAKYONDE

MSHIRIKI wa mkutano wa 39 wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), Musa Dube kutoka nchini Botswana ameishukuru na kuipongeza Taasisi ya MOI kwa huduma bora baada ya kupata matibabu ya ugonjwa uliokua unamsumbua.

Dube ametoa keki ya shukrani kwa taasisi ya MOI kama sehemu ya shukrani  na kuridhishwa na huduma bora alizopata. Keki hiyo ilikua na maneno “Thank you MOI” yenye maana ya ahsante MOI pamoja na bendera ya Botswana.

Aidha, Dube alikabidhi keki hiyo kwa Mkurugenzi Mtendaji wa MOI Dk. Respicious Boniface huku jopo la wataalamu waliomhudumia likishuhudia ambapo alitoa shukrani za dhati kwa huduma bora alizopata.

“Sidhani kama maneno yanaweza kutosheleza shukrani zangu , Ahsanteni sana kwa huduma nzuri, kwakweli nimepata huduma vizuri, ahsante kwa kila aliyeshirkiki kunitibu kuanzia mapokezi, Dk Shabani, Dk Mgisha, Dk Violeth, Elius, Patrick, Josephine na wengine wote, ahsanteni” Alisema.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa MOI Dk Respicious Boniface amemueleza Bi Dube kwamba MOI imekua ikitoa huduma kwa wananchi wa baadhi ya nchi za SADC hivyo kumuomba akawe balozi wa MOI nchini Botswana.

“Tunakushukuru sana kwa kuamua kurudi kutushukuru kwa kukuhudumia, tunaimani kubwa kwamba wapo wengine watakuja kutibiwa Tanzania kwasababu watasikia ulipata huduma bora hapa, wafikishie salamu waambie tuko tayari kuwahudumia pia” alisema Dk. Boniface.

Taasisi ya MOI imeshiriki katika maonyesho ya wiki ya viwanda pamoja na mkutano wa 39 wa nchi za SADC ambapo washiriki kutoka nchi mbalimbali wameshangazwa na huduma bora zinazotolewa na MOI kwa gharama nafuu ambazo hazipo kwenye nchi zao.

No comments:

Post a Comment

Pages